< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
The song of grecis `of Dauith. Israel seie now, No but for the Lord was in vs;
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
no but for `the Lord was in vs. Whanne men risiden vp ayens vs;
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
in hap thei hadden swalewid vs quike. Whanne the woodnesse of hem was wrooth ayens vs;
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
in hap watir hadde sope vs vp.
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
Oure soule passide thoruy a stronde; in hap oure soule hadde passide thoruy a watir vnsuffrable.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Blessid be the Lord; that `yaf not vs in taking to the teeth of hem.
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
Oure soule, as a sparowe, is delyuered; fro the snare of hunters. The snare is al to-brokun; and we ben delyuered.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Oure helpe is in the name of the Lord; that made heuene and erthe.

< Zaburi 124 >