< Zaburi 124 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
“A psalm of the steps, or the goings up. By David.” If the LORD had not been for us, Now may Israel say,
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
If the LORD had not been for us, When men rose up against us,
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
Then had they swallowed us up alive, When their wrath burned against us;
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
Then the waters had overwhelmed us; The stream had gone over our soul;
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
The proud waters had gone over our soul.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Blessed be the LORD, Who hath not given us a prey to their teeth!
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
We have escaped like a bird from the snare of the fowler; The snare is broken, and we have escaped.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Our help is in the name of the LORD, Who made heaven and earth.