< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
A Song of Degrees. If it had not been that the Lord was among us, let Israel now say;
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
if it had not been that the Lord was among us, when men rose up against us;
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
verily they would have swallowed us up alive, when their wrath was kindled against us:
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
verily the water would have drowned us, our soul would have gone under the torrent.
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
Yes, our soul would have gone under the overwhelming water.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Blessed be the Lord, who has not given us for a prey to their teeth.
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
Our soul has been delivered as a sparrow from the snare of the fowlers: the snare is broken, and we are delivered.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Our help is in the name of the Lord, who made heaven and earth.

< Zaburi 124 >