< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
A song for pilgrims going up to Jerusalem. A psalm of David. If the Lord hadn't been for us, what would have happened? Let everyone in Israel say:
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
If the Lord hadn't been for us, what would have happened when people came and attacked us?
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
They would have swallowed us alive when their anger raged against us.
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
Like a flood they would have swept over us; like a rushing torrent they would have submerged us.
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
They would have rushed over us like raging waters, drowning us.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Praise the Lord, who didn't hand us over to them as prey to be ripped apart by their teeth.
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
We escaped from them like a bird flying out of a hunter's trap. The trap was broken and we flew away!
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Our help comes from the Lord, who made heaven and earth.

< Zaburi 124 >