< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
En mi angustia, mi llanto subió al Señor, y él me dio una respuesta.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Oh Señor, sé el salvador de mi alma de los labios mentirosos y de la lengua del engaño.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
¿Qué castigo te dará? ¿Qué más te hará él, lengua falsa?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Flechas afiladas del fuerte y fuego ardiente.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
La aflicción es mía porque soy extraño en Mesec, y vivo en las tiendas de Cedar.
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Mi alma ha estado viviendo por mucho tiempo con los que odian la paz.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Estoy a favor de la paz; pero cuando digo eso, están a favor de la guerra.