< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Una canción de ascensos. En mi angustia, clamé a Yahvé. Me respondió.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Libera mi alma, Yahvé, de los labios mentirosos, de una lengua engañosa.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Lo que se te dará, y lo que se te hará más, ¿engañosa lengua?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Flechas afiladas de los poderosos, con carbones de enebro.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Ay de mí, que vivo en Meshech, ¡que habito entre las tiendas de Kedar!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Mi alma ha tenido su morada demasiado tiempo con el que odia la paz.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Estoy a favor de la paz, pero cuando hablo, son para la guerra.