< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Cántico gradual. A Yahvé clamé en medio de mi tribulación y Él me escuchó.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Yahvé, libra mi alma del labio engañoso, de la lengua astuta.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
¿Qué te dará o qué te añadirá (Yahvé), oh lengua astuta?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Saetas de un potente aguzadas en ascuas de retama.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
¡Ay de mí, advenedizo en Mósoc, alojado en las tiendas de Cedar!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Demasiado tiempo ha habitado mi alma entre los que odian la paz.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Yo soy hombre de paz; apenas hablo, y ellos mueven la guerra.

< Zaburi 120 >