< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
שיר המעלות אל-יהוה בצרתה לי-- קראתי ויענני
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
יהוה--הצילה נפשי משפת-שקר מלשון רמיה
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
מה-יתן לך ומה-יסיף לך-- לשון רמיה
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
חצי גבור שנונים עם גחלי רתמים
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
אויה-לי כי-גרתי משך שכנתי עם-אהלי קדר
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
רבת שכנה-לה נפשי-- עם שונא שלום
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
אני-שלום וכי אדבר המה למלחמה

< Zaburi 120 >