< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
ᾠδὴ τῶν ἀναβαθμῶν πρὸς κύριον ἐν τῷ θλίβεσθαί με ἐκέκραξα καὶ εἰσήκουσέν μου
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
κύριε ῥῦσαι τὴν ψυχήν μου ἀπὸ χειλέων ἀδίκων καὶ ἀπὸ γλώσσης δολίας
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
τί δοθείη σοι καὶ τί προστεθείη σοι πρὸς γλῶσσαν δολίαν
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
τὰ βέλη τοῦ δυνατοῦ ἠκονημένα σὺν τοῖς ἄνθραξιν τοῖς ἐρημικοῖς
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
οἴμμοι ὅτι ἡ παροικία μου ἐμακρύνθη κατεσκήνωσα μετὰ τῶν σκηνωμάτων Κηδαρ
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
πολλὰ παρῴκησεν ἡ ψυχή μου
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
μετὰ τῶν μισούντων τὴν εἰρήνην ἤμην εἰρηνικός ὅταν ἐλάλουν αὐτοῖς ἐπολέμουν με δωρεάν

< Zaburi 120 >