< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Ich rufe zu Jehovah in meiner Drangsal, und Er antwortet mir.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Jehovah, errette meine Seele von der Lüge Lippe, von der Zunge des Trugs.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Was gibt dir und was tut sie dir dazu, die Zunge des Trugs.
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Die Pfeile des Helden sind geschärft an den Glühkohlen des Wacholders.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Wehe mir, daß ich in Meschech mich aufhalte, daß ich wohne bei Kedars Zelten.
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Zu viel wohnt meine Seele bei dem, der Frieden haßt.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Ich bin für Frieden; aber wenn ich rede, sind sie für Krieg.

< Zaburi 120 >