< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Ein Wallfahrtslied. Ich rief zum HERRN in meiner Not, und er erhörte mich.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
HERR, rette meine Seele von den Lügenmäulern, von den falschen Zungen!
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Was kann dir anhaben und was noch weiter tun die falsche Zunge?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Sie ist wie scharfe Pfeile eines Starken aus glühendem Ginsterholz.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Wehe mir, daß ich in der Fremde zu Mesech weilen, daß ich bei den Zelten Kedars wohnen muß!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Lange genug hat meine Seele bei denen gewohnt, die den Frieden hassen!
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Ich bin für den Frieden; doch wenn ich rede, so sind sie für den Krieg.