< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Cantique graduel. A l'Éternel dans ma détresse j'élève mes cris, et Il m'exauce.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Éternel, délivre-moi des lèvres qui mentent, de la langue qui trompe!
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Que te donnera-t-Il, t'adjugera-t-Il, langue trompeuse?…
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Les traits acérés du guerrier, avec les charbons ardents du genêt.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Malheureux que je suis d'habiter en Mésech, de demeurer dans les tentes de Cédar!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Je n'ai que trop séjourné parmi ceux qui haïssent la paix.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Je ne veux que la paix; mais, si j'en parle, ils sont pour la guerre.