< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Cantique des degrés. À l’Éternel, en ma détresse, j’ai crié; et il m’a répondu.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Éternel! délivre mon âme de la lèvre menteuse, de la langue qui trompe.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Que te donnera-t-on, et que t’ajoutera-t-on, langue trompeuse? –
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Des flèches aiguës d’un homme puissant, et des charbons ardents de genêt.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Malheur à moi de ce que je séjourne en Méshec, de ce que je demeure avec les tentes de Kédar; –
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Que mon âme ait tant demeuré avec ceux qui haïssent la paix!
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Je veux la paix; mais si j’en parle, ils sont, eux, pour la guerre.

< Zaburi 120 >