< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
A song of ascents. In my distress I called out to Yahweh, and he answered me.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Rescue my life, Yahweh, from those who lie with their lips and deceive with their tongues.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
How will he punish you, and what more will he do to you, you who have a lying tongue?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
He will punish you with the arrows of a warrior sharpened over burning coals of the broom tree.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Woe is me because I temporarily live in Meshech; I lived previously among the tents of Kedar.
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
For too long I have lived with those who hate peace.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
I am for peace, but when I speak, they are for war.