< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
“A song of the degrees.” Unto the Lord, when I was in distress, did I call, and he hath answered me.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
O Lord, deliver my soul from lips of falsehood, and from a tongue of deceit.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
What will [God] give unto thee? or what will he add unto thee, thou tongue of deceit?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Sharpened arrows of the mighty, with coals of the broom-bush.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Woe is me, that I sojourn in Meshech, that I dwell in the tents of Kedar!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Too long for herself hath my soul dwelt with him that hateth peace.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
I am for peace; but when I speak, they are for war.