< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
A song for pilgrims going up to Jerusalem. I called out to the Lord for help in all my troubles, and he answered me.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Lord, please save me from liars and cheats!
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
What will the Lord do to you, you liars? How will he punish you?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
With the sharp arrows of a warrior and burning coals made from a broom tree.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
I'm sorry for myself, because I live as a foreigner in Meshech, or among the tent-dwellers of Kedar.
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
I have lived for far too long among people who hate peace.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
I want peace, but when I talk of peace, they want war.