< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
In my trouble I cried to the Lord: and he heard me.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
O Lord, deliver my soul from wicked lips, and a deceitful tongue.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
What shall be given to thee, or what shall be added to thee, to a deceitful tongue.
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
The sharp arrows of the mighty, with coals that lay waste.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Woe is me, that my sojourning is prolonged! I have dwelt with the inhabitants of cedar:
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
My soul hath been long a sojourner.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
With them that hate peace I was peaceable: when I spoke to them they fought against me without cause.

< Zaburi 120 >