< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
A Song of degrees. In my trouble I called unto Jehovah, and he answered me.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Jehovah, deliver my soul from the lying lip, from the deceitful tongue.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
What shall be given unto thee, what shall be added unto thee, thou deceitful tongue?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Sharp arrows of a mighty one, with burning coals of broom-wood.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Woe is me, that I sojourn in Meshech, that I dwell among the tents of Kedar!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
My soul hath long dwelt with them that hate peace.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
I [am for] peace; but when I speak, they [are] for war.