< Zaburi 120 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Píseň stupňů. K Hospodinu v ssoužení svém volal jsem, a vyslyšel mne.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Hospodine, vysvoboď duši mou od rtů lživých, a od jazyka lstivého.
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Coť prospěje, aneb coť přidá jazyk lstivý,
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Podobný k střelám přeostrým silného, a k uhlí jalovcovému?
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Běda mně, že pohostinu býti musím v Mešech, a přebývati v saláších Cedarských.
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Dlouho bydlí duše má mezi těmi, kteříž nenávidí pokoje.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Já ku pokoji, ale když mluvím, oni k boji.