< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
上行(或作登阶,下同)之诗。 我在急难中求告耶和华, 他就应允我。
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
耶和华啊,求你救我脱离说谎的嘴唇和诡诈的舌头!
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
诡诈的舌头啊,要给你什么呢? 要拿什么加给你呢?
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
就是勇士的利箭和罗腾木 的炭火。
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
我寄居在米设, 住在基达帐棚之中,有祸了!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
我与那恨恶和睦的人许久同住。
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
我愿和睦, 但我发言,他们就要争战。

< Zaburi 120 >