< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
Amo a Yavé, Porque escucha mi voz y mis súplicas,
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Porque inclina a mí su oído. Por tanto, [lo] invocaré mientras viva.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
Me rodearon las ataduras de la muerte. Me cayeron los terrores del Seol. Hallé angustia y tristeza. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Entonces invoqué el Nombre de Yavé: Oh Yavé, te busco, libra mi alma.
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Bondadoso y justo es Yavé. Sí, misericordioso es nuestro ʼElohim.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Yavé guarda a los sencillos. Estaba yo postrado Y Él me salvó.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
Vuelve, alma mía, a tu reposo, Porque Yavé te llenó de bien.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
Tú libraste mi vida de la muerte, Mis ojos, de las lágrimas, Y mis pies, de tropezar.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
Andaré delante de Yavé En la tierra de los vivientes.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
Creí, por tanto hablé: Estoy afligido en gran manera.
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
Y dije en mi apresuramiento: Todo hombre es mentiroso.
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
¿Qué pagaré a Yavé Por todos sus beneficios para mí?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
Levantaré la copa de la salvación E invocaré el Nombre de Yavé.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
A Yavé cumpliré mis votos En presencia de todo su pueblo.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Estimada es a los ojos de Yavé La muerte de sus santos.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Oh Yavé, ciertamente yo soy tu esclavo. Esclavo tuyo soy, hijo de tu esclava, Tú desataste mis ataduras.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
Te ofreceré sacrificio de acción de gracias E invocaré el Nombre de Yavé.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
A Yavé cumpliré mis votos, En presencia de todo su pueblo,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
En los patios de la Casa de Yavé, En medio de [ti], oh Jerusalén. ¡Aleluya!

< Zaburi 116 >