< Zaburi 113 >

1 Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Hvalite, sluge Gospodnje, hvalite ime Gospodnje,
2 Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Da bude ime Gospodnje blagosloveno otsad i dovijeka.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Od istoka sunèanoga do zapada da se slavi ime Gospodnje.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
Uzvišen je nad svima narodima Gospod; svrh nebesa je slava njegova.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
Ko je kao Gospod, Bog naš, koji sjedi na visini;
6 ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
Koji se sagiba da vidi što je na nebesima i na zemlji;
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
Koji iz praha podiže ubogoga, i iz kala uzvišuje ništega;
8 huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
I posaðuje ga s knezovima, s knezovima u narodu njegovu;
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.
Od nerotkinje naseljava kuæu, uèinivši je radosnom majkom sinovima. Aliluja!

< Zaburi 113 >