< Zaburi 104 >
1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
¡Qué todo mi ser alabe al Señor! ¡Dios mío, eres tan grande, revestido en majestad y esplendor!
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Usas la luz como vestidura; tú extiendes el tejido de los cielos.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Colocas las vigas de tu casa en las nubes de lluvia. Haces de las nubes de los cielos tus carruajes. Te montas sobre las alas del viento.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Haces de los vientos tus ángeles, y a las llamas de fuego tus sirvientes.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Tú pusiste la tierra sobre sus bases; y nunca será estremecida.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Estaba cubierta con océanos profundos, las aguas cubrían las montañas—
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
pero a tu orden las aguas huyeron; al sonido de tu trueno corren.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Las montañas se levantaron y los valles se hundieron hasta donde tú habías determinado.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Pusiste un límite para los océanos, para que no regresaran y volvieran a cubrir la tierra.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Haces que los manantiales fluyan hacia los arroyos, bajando desde las montañas.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Proveen agua para todos los animales salvajes, para que los caballos salvajes aplaquen su sed.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Los pájaros construyen sus nidos entre los árboles al lado de las corrientes de agua, cantando entre el follaje.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Envías lluvias sobre las montañas desde tu hogar en lo más alto; llenas la tierra con cosas buenas.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Haces que la grama crezca para las vacas, y las plantas también para que la gente se alimente de ellas, cultivos de la tierra para servir como alimento,
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
y vino para hacerlos felices, aceite de oliva para hacer resplandecer sus rostros, y pan para hacerlos fuertes.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Los árboles del Señor están bien regados, los cedros del líbano que Él plantó.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Los gorriones se anidan ahí; las garzas hacen sus nidos en los más altos árboles.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Las cabras salvajes viven en los picos de las montañas; y los damanes se esconden entre las rocas.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Tú hiciste la luna para marcar los meses, y el sol sabe cuándo ponerse.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Haces caer la oscuridad para que venga la noche, el momento en el que los animales del bosque salen a cazar.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Los jóvenes leones rugen mientras buscan a su presa, buscando la comida que Dios les proveyó.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Cuando el sol sale vuelven a sus guaridas para descansar.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Entonces las personas salen a hacer sus tareas, y trabajan hasta el ocaso.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Señor, ¡Cuántas cosas has hecho, todas ellas sabiamente formadas! La tierra está llena de tus criaturas.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Considera el mar, profundo y ancho, lleno de todos los tipos de seres vivientes, grandes y pequeños.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Los barcos navegan allí, y el Leviatán, que creaste para que jugara en él.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Todas las criaturas te buscan para que les des comida en el momento correcto.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Cuando se las provees, la recogen. Les repartes alimento a todos, y son saciados.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Cuando te alejas de ellos, se aterrorizan; cuando retiras su aliento de vida, ellos mueren y regresan al polvo.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Mas cuando envías tu aliento, son creados, y la vida cubre la tierra una vez más.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
¡Qué la gloria del Señor permanezca para siempre! El Señor se alegra con todo lo que ha hecho.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Solo tiene que mirar hacia la tierra y esta tiembla; las montañas dejan salir humo a su toque.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Cantaré al Señor mientras viva; cantaré alabanzas a Dios toda mi vida.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Ojalá el Señor se plazca con mis pensamientos porque me alegro en el Señor.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
¡Sean destruidos los pecadores de la tierra; qué los malvados dejen de existir! ¡Todo mi ser alabe al Señor!