< Zaburi 102 >

1 Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
Preghiera di un afflitto che è stanco e sfoga dinanzi a Dio la sua angoscia. Signore, ascolta la mia preghiera, a te giunga il mio grido.
2 Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
Non nascondermi il tuo volto; nel giorno della mia angoscia piega verso di me l'orecchio. Quando ti invoco: presto, rispondimi.
3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
Si dissolvono in fumo i miei giorni e come brace ardono le mie ossa.
4 Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
Il mio cuore abbattuto come erba inaridisce, dimentico di mangiare il mio pane.
5 Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
Per il lungo mio gemere aderisce la mia pelle alle mie ossa.
6 Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
Sono simile al pellicano del deserto, sono come un gufo tra le rovine.
7 Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
Veglio e gemo come uccello solitario sopra un tetto.
8 Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
Tutto il giorno mi insultano i miei nemici, furenti imprecano contro il mio nome.
9 Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
Di cenere mi nutro come di pane, alla mia bevanda mescolo il pianto,
10 kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
davanti alla tua collera e al tuo sdegno, perché mi sollevi e mi scagli lontano.
11 Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
I miei giorni sono come ombra che declina, e io come erba inaridisco.
12 Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
Ma tu, Signore, rimani in eterno, il tuo ricordo per ogni generazione.
13 Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
Tu sorgerai, avrai pietà di Sion, perché è tempo di usarle misericordia: l'ora è giunta.
14 Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
Poiché ai tuoi servi sono care le sue pietre e li muove a pietà la sua rovina.
15 Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
I popoli temeranno il nome del Signore e tutti i re della terra la tua gloria,
16 Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
quando il Signore avrà ricostruito Sion e sarà apparso in tutto il suo splendore.
17 Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
Egli si volge alla preghiera del misero e non disprezza la sua supplica.
18 Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
Questo si scriva per la generazione futura e un popolo nuovo darà lode al Signore.
19 “Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
Il Signore si è affacciato dall'alto del suo santuario, dal cielo ha guardato la terra,
20 kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
per ascoltare il gemito del prigioniero, per liberare i condannati a morte;
21 Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
perché sia annunziato in Sion il nome del Signore e la sua lode in Gerusalemme,
22 wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
quando si aduneranno insieme i popoli e i regni per servire il Signore.
23 Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
Ha fiaccato per via la mia forza, ha abbreviato i miei giorni.
24 Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
Io dico: Mio Dio, non rapirmi a metà dei miei giorni; i tuoi anni durano per ogni generazione.
25 Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
In principio tu hai fondato la terra, i cieli sono opera delle tue mani.
26 Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
Essi periranno, ma tu rimani, tutti si logorano come veste, come un abito tu li muterai ed essi passeranno.
27 Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
Ma tu resti lo stesso e i tuoi anni non hanno fine.
28 Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
I figli dei tuoi servi avranno una dimora, resterà salda davanti a te la loro discendenza.

< Zaburi 102 >