< Mithali 4 >

1 Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
OID, hijos, la doctrina de un padre, y estad atentos para que conozcáis cordura.
2 Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
Porque os doy buena enseñanza; no desamparéis mi ley.
3 Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
Porque yo fuí hijo de mi padre, delicado y único delante de mi madre.
4 baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
Y él me enseñaba, y me decía: Mantenga tu corazón mis razones, guarda mis mandamientos, y vivirás:
5 Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
Adquiere sabiduría, adquiere inteligencia; no te olvides ni te apartes de las razones de mi boca;
6 Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
No la dejes, y ella te guardará; ámala, y te conservará.
7 Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
Sabiduría ante todo: adquiere sabiduría: y ante toda tu posesión adquiere inteligencia.
8 Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
Engrandécela, y ella te engrandecerá: ella te honrará, cuando tú la hubieres abrazado.
9 Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
Adorno de gracia dará á tu cabeza: corona de hermosura te entregará.
10 Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
Oye, hijo mío, y recibe mis razones; y se te multiplicarán años de vida.
11 Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
Por el camino de la sabiduría te he encaminado, y por veredas derechas te he hecho andar.
12 Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
Cuando anduvieres no se estrecharán tus pasos; y si corrieres, no tropezarás.
13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
Ten el consejo, no lo dejes; guárdalo, porque eso es tu vida.
14 Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
No entres por la vereda de los impíos, ni vayas por el camino de los malos.
15 Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
Desampárala, no pases por ella; apártate de ella, pasa.
16 Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
Porque no duermen ellos, si no hicieren mal; y pierden su sueño, si no han hecho caer.
17 Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
Porque comen pan de maldad, y beben vino de robos.
18 Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
Mas la senda de los justos es como la luz de la aurora, que va en aumento hasta que el día es perfecto.
19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
El camino de los impíos es como la oscuridad: no saben en qué tropiezan.
20 Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
Hijo mío, está atento á mis palabras; inclina tu oído á mis razones.
21 Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
No se aparten de tus ojos; guárdalas en medio de tu corazón.
22 kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
Porque son vida á los que las hallan, y medicina á toda su carne.
23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
Sobre toda cosa guardada guarda tu corazón; porque de él mana la vida.
24 Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
Aparta de ti la perversidad de la boca, y aleja de ti la iniquidad de labios.
25 Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
Tus ojos miren lo recto, y tus párpados en derechura delante de ti.
26 Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
Examina la senda de tus pies, y todos tus caminos sean ordenados.
27 Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.
No te apartes á diestra, ni á siniestra: aparta tu pie del mal.

< Mithali 4 >