< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Mon fils, n'oublie point mon enseignement, et que ton cœur garde mes commandements.
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Car ils t'apporteront de longs jours, et des années de vie, et la prospérité.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Que la miséricorde et la vérité ne t'abandonnent point; lie-les à ton cou, écris-les sur la table de ton cœur;
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Et tu obtiendras la grâce et une grande sagesse aux yeux de Dieu et des hommes.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Confie-toi en l'Éternel de tout ton cœur, et ne t'appuie point sur ta prudence.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
Considère-le dans toutes tes voies, et il dirigera tes sentiers.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Ne sois point sage à tes propres yeux; crains l'Éternel, et détourne-toi du mal.
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
Ce sera la santé pour tes muscles et un rafraîchissement pour tes os.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Honore l'Éternel de ton bien, et des prémices de tout ton revenu;
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
Et tes greniers seront remplis d'abondance, et tes cuves regorgeront de moût.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
Mon fils, ne rejette point la correction de l'Éternel, et ne perds pas courage de ce qu'il te reprend;
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Car l'Éternel châtie celui qu'il aime, comme un père l'enfant qu'il chérit.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Heureux l'homme qui a trouvé la sagesse, et l'homme qui avance dans l'intelligence!
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
Car il vaut mieux l'acquérir que de gagner de l'argent, et le revenu qu'on en peut tirer vaut mieux que l'or fin.
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
Elle est plus précieuse que les perles, et toutes les choses désirables ne la valent pas.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Il y a de longs jours dans sa droite, des richesses et de la gloire dans sa gauche.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Ses voies sont des voies agréables, et tous ses sentiers conduisent à la paix.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
Elle est l'arbre de vie pour ceux qui l'embrassent, et tous ceux qui la conservent sont rendus bienheureux.
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
L'Éternel a fondé la terre par la sagesse, et agencé les cieux par l'intelligence.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
C'est par sa science que les abîmes s'ouvrent, et que les nuées distillent la rosée.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
Mon fils, qu'elles ne s'écartent point de devant tes yeux; garde la sagesse et la prudence,
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
Et elles seront la vie de ton âme, et un ornement à ton cou.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Alors tu marcheras en assurance par ton chemin, et ton pied ne heurtera point.
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
Si tu te couches, tu n'auras point de frayeur; et quand tu seras couché, ton sommeil sera doux.
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
Ne crains point la frayeur soudaine, ni l'attaque des méchants, quand elle arrivera.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
Car l'Éternel sera ton espérance, et il gardera ton pied du piège.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
Ne refuse pas un bienfait à celui qui en a besoin, quand il est en ton pouvoir de l'accorder.
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
Ne dis point à ton prochain: Va et reviens, et je te donnerai demain; quand tu as de quoi donner.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Ne machine point de mal contre ton prochain qui habite en assurance avec toi.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
N'aie point de procès sans sujet avec personne, lorsqu'on ne t'a fait aucun mal.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Ne porte pas envie à l'homme violent, et ne choisis aucune de ses voies.
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Car celui qui va de travers est en abomination à l'Éternel; mais il est l'ami de ceux qui sont droits.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
La malédiction de l'Éternel est dans la maison du méchant; mais il bénit la demeure des justes.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Il se moque des moqueurs; mais il fait grâce aux humbles.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Les sages hériteront la gloire; mais l'ignominie accablera les insensés.

< Mithali 3 >