< Mithali 2 >

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
son: child my if to take: recieve word my and commandment my to treasure with you
2 kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
to/for to listen to/for wisdom ear your to stretch heart your to/for understanding
3 na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
that if: except if: except to/for understanding to call: call out to/for understanding to give: cry out voice your
4 na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
if to seek her like/as silver: money and like/as treasure to search her
5 ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
then to understand fear LORD and knowledge God to find
6 Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
for LORD to give: give wisdom from lip his knowledge and understanding
7 Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
(to treasure *Q(K)*) to/for upright wisdom shield to/for to go: walk integrity
8 kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
to/for to watch way justice and way: journey (pious his *Q(K)*) to keep: guard
9 Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
then to understand righteousness and justice and uprightness all track good
10 Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
for to come (in): come wisdom in/on/with heart your and knowledge to/for soul your be pleasant
11 Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
plot to keep: guard upon you understanding to watch you
12 Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
to/for to rescue you from way: conduct bad: evil from man: anyone to speak: speak perversity
13 wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
[the] to leave: forsake way uprightness to/for to go: walk in/on/with way: conduct darkness
14 wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
[the] glad to/for to make: do bad: evil to rejoice in/on/with perversity bad: evil
15 ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
which way their twisted and be devious in/on/with track their
16 Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
to/for to rescue you from woman be a stranger from foreign word her to smooth
17 aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
[the] to leave: forsake tame youth her and [obj] covenant God her to forget
18 Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
for to sink to(wards) death house: home her and to(wards) shade track her
19 Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
all to come (in): come her not to return: return [emph?] and not to overtake way life
20 Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
because to go: walk in/on/with way: conduct pleasant and way righteous to keep: obey
21 Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
for upright (to dwell *L(bah)*) land: country/planet and unblemished: blameless to remain in/on/with her
22 Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
and wicked from land: country/planet to cut: eliminate and to act treacherously to pull from her

< Mithali 2 >