< Wafilipi 1 >
1 Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
Paulus og Timotheus, Kristi Jesu Tjenere, til alle de hellige i Kristus Jesus, som ere i Filippi, med Tilsynsmænd og Menighedstjenere.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Naade være med eder og Fred fra Gud vor Fader og den Herre Jesus Kristus!
3 Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
Jeg takker min Gud, saa ofte jeg kommer eder i Hu,
4 Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
idet jeg altid, i hver min Bøn, beder for eder alle med Glæde,
5 kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
for eders Deltagelse i Evangeliet fra den første Dag indtil nu;
6 Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
forvisset om dette, at han, som begyndte en god Gerning i eder, vil fuldføre den indtil Jesu Kristi Dag,
7 Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
saaledes som det jo er ret for mig at mene dette om eder alle, efterdi jeg har eder i Hjertet baade under mine Lænker og under Evangeliets Forsvar og Stadfæstelse, fælles som I jo alle ere med mig om Naaden.
8 Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
Thi Gud er mit Vidne, hvorledes jeg længes efter eder alle med Kristi Jesu inderlige Kærlighed.
9 Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
Og derom beder jeg, at eders Kærlighed fremdeles maa blive mere og mere rig paa Erkendelse og al Skønsomhed,
10 ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
saa I kunne værdsætte de forskellige Ting, for at I maa være rene og uden Anstød til Kristi Dag,
11 mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
fyldte med Retfærdigheds Frugt, som virkes ved Jesus Kristus, Gud til Ære og Pris.
12 Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
Men jeg vil, I skulle vide, Brødre! at mine Forhold snarere have tjent til Evangeliets Fremme,
13 Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
saa at det er blevet aabenbart for hele Livvagten og for alle de øvrige, at mine Lænker bæres for Kristi Skyld,
14 Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
og de fleste af Brødrene fik i Tillid til Herren ved mine Lænker end mere Dristighed til at tale Guds Ord uden Frygt.
15 Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
Nogle prædike vel ogsaa Kristus for Avinds og Kivs Skyld, men nogle ogsaa i en god Mening.
16 Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
Disse gøre det af Kærlighed, vidende, at jeg er sat til at forsvare Evangeliet;
17 Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
men hine forkynde Kristus af Egennytte, ikke ærligt, men i den Tanke at føje Trængsel til mine Lænker.
18 Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
Hvad saa? Kristus forkyndes dog paa enhver Maade, være sig paa Skrømt eller i Sandhed; og derover glæder jeg mig, og jeg vil ogsaa fremdeles glæde mig.
19 kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
Thi jeg ved, at dette skal blive mig til Frelse ved eders Bøn og Jesu Kristi Aands Hjælp,
20 Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
efter min Længsel og mit Haab, at jeg i intet skal blive til Skamme, men at Kristus skal med al Frimodighed, som altid, saa ogsaa nu, forherliges i mit Legeme, være sig ved Liv eller ved Død.
21 Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Thi det at leve er mig Kristus og at dø en Vinding.
22 Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
Men dersom dette at leve i Kødet skaffer mig Frugt af min Gerning, saa ved jeg ikke, hvad jeg skal vælge;
23 Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
men jeg staar tvivlraadig imellem de to Ting, idet jeg har Lysten til at bryde op og være sammen med Kristus; thi dette var saare meget bedre;
24 Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
men at forblive i Kødet er mere nødvendigt for eders Skyld.
25 Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
Og i Forvisning herom ved jeg, at jeg skal blive i Live og forblive hos eder alle til eders Fremgang og Glæde i Troen,
26 Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
for at eders Ros ved mig kan blive rig i Kristus Jesus, ved at jeg atter kommer til Stede iblandt eder.
27 Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
Kun skulle I leve Kristi Evangelium værdigt, for at, hvad enten jeg kommer og ser eder eller er fraværende, jeg dog kan høre om eder, at I staa faste i een Aand, saa at I med een Sjæl stride tilsammen for Troen paa Evangeliet
28 wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
og ikke lade eder forfærde i nogen Ting af Modstanderne; thi dette er for dem et Tegn paa Undergang, men for eder paa Frelse, og det fra Gud.
29 Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
Thi eder er det forundt for Kristi Skyld — ikke alene at tro paa ham, men ogsaa at lide for hans Skyld,
30 kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.
idet I have den samme Kamp, som I have set paa mig og nu høre om mig.