< Hesabu 9 >

1 Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
İsrailliler'in Mısır'dan çıkışlarının ikinci yılının birinci ayında RAB Sina Çölü'nde Musa'ya şöyle seslendi:
2 “Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
“İsrailliler Fısıh kurbanını belirlenen zamanda kessinler.
3 Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
Bütün kurallar, ilkeler uyarınca kurbanı belirlenen zamanda, bu ayın on dördüncü gününün akşamüstü keseceksiniz.”
4 Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
Böylece Musa İsrailliler'e Fısıh kurbanını kesmelerini söyledi.
5 nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Onlar da Sina Çölü'nde birinci ayın on dördüncü gününün akşamüstü Fısıh kurbanını kestiler. Her şeyi RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
6 Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile,
Ancak, ölüye dokunduklarından kirli sayılan bazı kişiler o gün Fısıh kurbanını kesemediler. Aynı gün Musa'yla Harun'a gelip
7 wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”
Musa'ya, “Ölüye dokunduğumuzdan kirli sayılırız” dediler, “Ama öbür İsrailliler'le birlikte belirlenen zamanda RAB'bin sunusunu sunmamız neden engellensin?”
8 Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”
Musa, “RAB'bin sizinle ilgili bana neler söyleyeceğini duyuncaya dek bekleyin” dedi.
9 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
10 “Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana.
“İsrailliler'e de ki, ‘Sizlerden ya da soyunuzdan ölüye dokunduğu için kirli sayılan ya da uzak bir yolculukta bulunan biri RAB'bin Fısıh kurbanını kesebilir.
11 Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu.
İkinci ayın on dördüncü gününün akşamüstü Fısıh kurbanını kesip mayasız ekmek ve acı otlarla yiyecek.
12 Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote.
Sabaha dek kurbandan bir şey bırakmayacak, kemiklerini kırmayacak. Fısıh kurbanını bütün kuralları uyarınca kesmelidir.
13 Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.
Ancak, temiz sayılan ve yolculukta olmayan biri Fısıh kurbanını kesmeyi savsaklarsa, halkının arasından atılacaktır. Çünkü belirlenen zamanda RAB'bin sunusunu sunmamıştır. Günahının cezasını çekecektir.
14 “‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’”
“‘Aranızda yaşayan bir yabancı RAB'bin Fısıh kurbanını kesmek isterse, Fısıh'ın kuralları, ilkeleri uyarınca kesmelidir. Yerli ya da yabancı için aynı kuralı uygulamalısınız.’”
15 Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto.
Konut, yani Levha Sandığı'nın bulunduğu çadır kurulduğu gün üstünü bulut kapladı. Konutun üstündeki bulut akşamdan sabaha dek ateşi andırdı.
16 Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto.
Bu hep böyle sürüp gitti. Konutu kaplayan bulut gece ateşi andırıyordu.
17 Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi.
İsrailliler ancak bulut çadırın üzerinden kalkınca göçer, bulut nerede durursa orada konaklarlardı.
18 Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.
RAB'bin buyruğu uyarınca göç eder, yine RAB'bin buyruğu uyarınca konaklarlardı. Bulut konutun üzerinde durdukça yerlerinden ayrılmazlardı.
19 Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka.
Bulut konutun üzerinde uzun süre durduğu zaman RAB'bin buyruğuna uyar, yola çıkmazlardı.
20 Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.
Bazen bulut konutun üzerinde birkaç gün kalırdı. Halk da RAB'bin verdiği buyruğa göre ya konakladığı yerde kalır ya da göç ederdi.
21 Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka.
Bazı günler bulut akşamdan sabaha dek kalır, sabah konutun üzerinden kalkar kalkmaz halk yola çıkardı. Gece olsun, gündüz olsun, bulut konutun üzerinden kalkar kalkmaz halk yola çıkardı.
22 Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.
Bulut konutun üzerinde iki gün, bir ay ya da uzun süre kalsa bile, İsrailliler konakladıkları yerde kalır, yola koyulmazlardı. Ama bulut kalkar kalkmaz yola çıkarlardı.
23 Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.
RAB'bin buyruğu uyarınca konaklar ya da yola çıkarlardı. Böylece RAB'bin Musa aracılığıyla verdiği buyruğa uydular.

< Hesabu 9 >