< Hesabu 10 >
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
“Dövme gümüşten iki borazan yapacaksın; bunları topluluğu çağırmak ve halkın yola çıkması için kullanacaksın.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
İki borazan birden çalınınca, bütün topluluk senin yanında, Buluşma Çadırı'nın girişi önünde toplanacak.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Yalnız biri çalınırsa, önderler, İsrail'in oymak başları senin yanında toplanacak.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Borazan kısa çalınınca, doğuda konaklayanlar yola çıkacak.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
İkinci kez kısa çalınınca da güneyde konaklayanlar yola çıkacak. Borazanın kısa çalınması oymakların yola çıkması için bir işarettir.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Topluluğu toplamak için de borazan çaldırt, ama kısa olmasın.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
“Borazanları kâhin olan Harunoğulları çalacak. Borazan çalınması sizler ve gelecek kuşaklar için kalıcı bir kural olacak.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Sizi sıkıştıran düşmana karşı ülkenizde savaşa çıktığınızda, borazan çalın. O zaman Tanrınız RAB sizi anımsayacak, sizi düşmanlarınızdan kurtaracak.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Sevinçli olduğunuz günler –kutladığınız bayramlar ve Yeni Ay Törenleri'nde– yakmalık sunular ve esenlik kurbanları üzerine borazan çalacaksınız. Böylelikle Tanrınız'ın önünde anımsanmış olacaksınız. Ben Tanrınız RAB'bim.”
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
İkinci yılın ikinci ayının yirminci günü bulut Levha Sandığı'nın bulunduğu konutun üzerinden kalktı.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
İsrailliler de Sina Çölü'nden göç etmeye başladılar. Bulut Paran Çölü'nde durdu.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Bu, RAB'bin Musa aracılığıyla verdiği buyruk uyarınca ilk göç edişleriydi.
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
Önce Yahuda sancağı bölükleriyle yola çıktı. Yahuda bölüğüne Amminadav oğlu Nahşon komuta ediyordu.
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
İssakar oymağının bölüğüne Suar oğlu Netanel,
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Zevulun oymağının bölüğüne de Helon oğlu Eliav komuta ediyordu.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
Konut yere indirilince, onu taşıyan Gerşonoğulları'yla Merarioğulları yola koyuldular.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Sonra Ruben sancağı bölükleriyle yola çıktı. Ruben bölüğüne Şedeur oğlu Elisur komuta ediyordu.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Şimon oymağının bölüğüne Surişadday oğlu Şelumiel,
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
Gad oymağının bölüğüne de Deuel oğlu Elyasaf komuta ediyordu.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Kehatlılar kutsal eşyaları taşıyarak yola koyuldular. Bunlar varmadan konut kurulmuş olurdu.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Efrayim sancağı bölükleriyle yola çıktı. Efrayim bölüğüne Ammihut oğlu Elişama komuta ediyordu.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Manaşşe oymağının bölüğüne Pedahsur oğlu Gamliel,
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
Benyamin oymağının bölüğüne de Gidoni oğlu Avidan komuta ediyordu.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
En sonunda Dan sancağı ordunun artçı kolu olan bölükleriyle yola çıktı. Dan bölüğüne Ammişadday oğlu Ahiezer komuta ediyordu.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Aşer oymağının bölüğüne Okran oğlu Pagiel,
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Naftali oymağının bölüğüne de Enan oğlu Ahira komuta ediyordu.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Yola koyulduklarında İsrailli bölüklerin yürüyüş düzeni böyleydi.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Musa, kayınbabası Midyanlı Reuel oğlu Hovav'a, “RAB'bin, ‘Size vereceğim’ dediği yere gidiyoruz” dedi, “Bizimle gel, sana iyi davranırız. Çünkü RAB İsrail'e iyilik edeceğine söz verdi.”
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Hovav, “Gelmem” diye yanıtladı, “Ülkeme, akrabalarımın yanına döneceğim.”
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Musa, “Lütfen bizi bırakma” diye üsteledi, “Çünkü çölde konaklayacağımız yerleri sen biliyorsun. Sen bize göz olabilirsin.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Bizimle gelirsen, RAB'bin yapacağı bütün iyilikleri seninle paylaşırız.”
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
RAB'bin Dağı'ndan ayrılıp üç günlük yol aldılar. Konaklayacakları yeri bulmaları için RAB'bin Antlaşma Sandığı üç gün boyunca önleri sıra gitti.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Konakladıkları yerden ayrıldıklarında da RAB'bin bulutu gündüzün onların üzerinde duruyordu.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Sandık yola çıkınca Musa, “Ya RAB, kalk! Düşmanların dağılsın, Senden nefret edenler önünden kaçsın!” diyordu.
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Sandık konaklayınca da, “Ya RAB, binlerce, on binlerce İsrailli'ye dön!” diyordu.