< Mika 3 >
1 Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
And I said: Listen, leaders of Jacob and chiefs of the house of Israel. Does it not belong to you to know judgment,
2 ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
you who hold hatred for good, and love evil, who violently steal their skins from over them and their flesh from over their bones?
3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
They have devoured the flesh of my people, and have stripped their skin from over them, and they have shattered and chopped their bones, as if for the kettle, and like flesh in the middle of the pot.
4 Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
Then they will cry out to the Lord, and he will not heed them. And he will hide his face from them in that time, just as they have acted wickedly with their inventions.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
Thus says the Lord about the prophets who seduce my people: They bite with their teeth and preach peace, and if anyone does not give something to their mouth, they sanctify a battle against him.
6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
Because of this, night will be yours for vision, and darkness yours for divination, and the sun will meet with death over the prophets, and the day will be darkened over them.
7 Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
And those who see visions will be confounded, and the diviners will be confounded. And they will all cover their faces, because there is no response from God.
8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Nevertheless, truly I have been filled with the strength of the Spirit of the Lord, with judgment and virtue, in order to announce to Jacob his wickedness and to Israel his sin.
9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
Hear this, leaders of the house of Jacob and judges of the house of Israel, you who abominate judgment and who pervert all that is right.
10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
You build up Zion with blood, and Jerusalem with iniquity.
11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
Her leaders have judged for tributes, and her priests have taught for payment, and her prophets divined for money. And they leaned upon the Lord, saying: “Is not the Lord in our midst? No disaster will overcome us.”
12 Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.
For this reason, because of you, Zion will be plowed under like a field, and Jerusalem will become like a pile of stones, and the mountain of the temple like the high places of the forests.