< Nahumu 1 >
1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
The burden of Nineveh. The book of the vision of Nahum the Elkoshite.
2 Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
God is a rival, and the Lord is avenging. The Lord is avenging, and one who applies wrath. The Lord is avenging with his enemies, and he becomes angry with his adversaries.
3 Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
The Lord is patient and great in strength, and those who are not clean, he makes innocent. The Lord is in a tempest, and his way is a whirlwind, and the clouds are dust at his feet.
4 Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
He is the one who rebukes the sea, and who dries it up, and who leads all the rivers to the desert. Basan has been weakened, and also Carmel, and the flower of Lebanon has languished.
5 Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
The mountains have trembled before him, and the hills have become desolate, and the earth has quaked before his face, both the world and all that dwells in it.
6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
Who can stand firm before the face of his indignation? And who can continue against the fury of his wrath? His indignation has broken out like a fire, and the rocks have been dissolved before him.
7 Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
The Lord is good, and a comforter in the day of tribulation, and he knows those who hope in him.
8 lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
And in the flood that passes over, he brings to consummation the end of his place. And darkness shall pursue his adversaries.
9 Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
What are you thinking up against the Lord? He will accomplish the consummation. There shall not rise up a double tribulation.
10 Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
For just as thorns entwine one another, so also, while they are feasting and drinking together, they will be consumed like stubble that is completely dry.
11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
Out of you will go forth one who thinks up evil against the Lord, dragging betrayals through his mind.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
Thus says the Lord: If they had been perfect, and many of them so, yet still they would be pruned, and it will cross through them. I have afflicted you, and I shall afflict you no more.
13 Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
And now I will shatter his rod from your back, and I will break open your bonds.
14 Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
And the Lord will place a commandment over you; nothing more from your name will be sown. From the house of your God, I will order destroyed the graven image and the molten image. I will prepare your grave, because you are not honorable.
15 Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.
Behold, over the mountains, the feet of the Evangelizer and the Announcer of peace. Judah, celebrate your festivals and keep your vows. For Belial will never again pass through you; he has completely passed away.