< Mathayo 4 >

1 Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
Then was Jesus led by the Spirit into the wilderness to be tempted by the devil.
2 Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
And when he had fasted forty days and forty nights, he was afterward hungry.
3 Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
And when the tempter came to him, he said, If thou art the Son of God, command that these stones be made bread.
4 Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
But he answered and said, It is written, Man shall not live by bread alone, but by every word that proceedeth out of the mouth of God.
5 Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
Then the devil taketh him up into the holy city, and setteth him on a pinnacle of the temple,
6 akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
And saith to him, If thou art the Son of God, cast thyself down: for it is written, He shall give his angels charge concerning thee: and in their hands they shall uphold, thee, lest at any time thou dash thy foot against a stone.
7 Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
Jesus said to him, It is written again, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
8 Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
Again, the devil taketh him up upon an exceeding high mountain, and showeth him all the kingdoms of the world, and the glory of them;
9 kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
And saith to him, All these things will I give thee, if thou wilt fall down and worship me.
10 Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
Then saith Jesus to him, Away with thee, Satan: for it is written, Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.
11 Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
Then the devil leaveth him, and, behold, angels came and ministered to him.
12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
Now when Jesus had heard that John was cast into prison, he departed into Galilee;
13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
And leaving Nazareth, he came and dwelt in Capernaum, which is upon the sea coast, in the borders of Zebulun and Naphtali:
14 ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
That it might be fulfilled which was spoken by Isaiah the prophet, saying,
15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
The land of Zebulun, and the land of Naphtali, by the way of the sea, beyond Jordan, Galilee of the Gentiles;
16 watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
The people who sat in darkness saw great light; and to them who sat in the region and shadow of death light hath shone.
17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
From that time Jesus began to preach, and to say, Repent: for the kingdom of heaven is at hand.
18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
And Jesus, walking by the sea of Galilee, saw two brethren, Simon called Peter, and Andrew his brother, casting a net into the sea: for they were fishermen.
19 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
And he saith to them, Follow me, and I will make you fishers of men.
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
And they immediately left their nets, and followed him.
21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
And going on from there, he saw other two brethren, James the son of Zebedee, and John his brother, in a boat with Zebedee their father, mending their nets; and he called them.
22 Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
And they immediately left the boat and their father, and followed him.
23 Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
And Jesus went about all Galilee, teaching in their synagogues, and preaching the gospel of the kingdom, and healing all manner of sickness and all manner of disease among the people.
24 Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
And his fame spread throughout all Syria: and they brought to him all sick people that were sick with various diseases and torments, and those who were possessed with demons, and those who were lunatic, and those that had the palsy; and he healed them.
25 Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.
And there followed him great multitudes of people from Galilee, and from Decapolis, and from Jerusalem, and from Judaea, and from beyond Jordan.

< Mathayo 4 >