< Marko 1 >
1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God;
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
As it is written in the prophets, Behold, I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee.
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths straight.
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
John was baptizing in the wilderness, and preaching the baptism of repentance for the remission of sins.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
And there went out to him all the land of Judaea, and they of Jerusalem, and were all baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
And John was clothed with camel’s hair, and with a leather belt around his loins; and he ate locusts and wild honey;
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
And preached, saying, There cometh after me one mightier than I, the latchet of whose shoes I am not worthy to stoop down and loose.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I indeed have baptized you in water: but he shall baptize you in the Holy Spirit.
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
And it came to pass in those days, that Jesus came from Nazareth to Galilee, and was baptized by John in Jordan.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
And immediately coming up out of the water, he saw the heavens opened, and the Spirit like a dove descending upon him:
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
And there came a voice from heaven, saying, Thou art my beloved Son, in whom I am well pleased.
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
And immediately the Spirit driveth him into the wilderness.
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
And he was there in the wilderness forty days, tempted by Satan; and was with the wild beasts; and the angels ministered to him.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
Now after John was put in prison, Jesus came into Galilee, preaching the gospel of the kingdom of God,
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
And saying, The time is fulfilled, and the kingdom of God is at hand: repent ye, and believe the gospel.
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
Now as he was walking by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew his brother casting a net into the sea: for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
And Jesus said to them, Come ye after me, and I will make you to become fishers of men.
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
And immediately they forsook their nets, and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And when he had gone a little further from there, he saw James the son of Zebedee, and John his brother, who also were in the boat mending their nets.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
And immediately he called them: and they left their father Zebedee in the boat with the hired servants, and went after him.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
And they went into Capernaum; and immediately on the sabbath he entered into the synagogue, and taught.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
And they were astonished at his doctrine: for he taught them as one that had authority, and not as the scribes.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
And there was in their synagogue a man with an unclean spirit; and he cried out,
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
Saying, Let us alone; what have we to do with thee, thou Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace, and come out of him.
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
And when the unclean spirit had torn him, and cried with a loud voice, he came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all amazed, so that they questioned among themselves, saying, What thing is this? what new doctrine is this? for with authority he commandeth even the unclean spirits, and they obey him.
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
And immediately his fame spread abroad throughout all the region surrounding Galilee.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
And immediately, when they had come out of the synagogue, they entered into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
But the mother of Simon’s wife lay sick with a fever, and immediately they tell him of her.
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
And he came and took her by the hand, and lifted her up; and immediately the fever left her, and she ministered to them.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
And at evening, when the sun had set, they brought to him all that were diseased, and them that were possessed with demons.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
And all the city was gathered together at the door.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
And he healed many that were sick with various diseases, and cast out many demons; and permitted not the demons to speak, because they knew him.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
And in the morning, rising a great while before day, he went out, and departed into a solitary place, and there prayed.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
And Simon and they that were with him followed after him.
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
And when they had found him, they said to him, All men seek for thee.
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
And he said to them, Let us go into the next towns, that I may preach there also: for this purpose have I come.
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
And he preached in their synagogues throughout all Galilee, and cast out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
And there came a leper to him, beseeching him, and kneeling down to him, and saying to him, If thou wilt, thou canst make me clean.
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
And Jesus, moved with compassion, put forth his hand, and touched him, and saith to him, I will; be thou clean.
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
And as soon as he had spoken, immediately the leprosy departed from him, and he was cleansed.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
And he strictly charged him, and immediately sent him away;
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
And saith to him, See thou say nothing to any man: but go, show thyself to the priest, and offer for thy cleansing those things which Moses commanded, for a testimony to them.
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
But he went out, and began to proclaim it freely, and to blaze abroad the matter, so that Jesus could no more openly enter into the city, but was without in desert places: and they came to him from every quarter.