< Luka 9 >

1 Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
Aru jitia Jisu baroh jon chela khan ke matise, Tai pora chela khan ke bhoot khan ke kheda bole aru bemar ke bhal kori bole laga hokti aru adhikar dise,
2 kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
aru Tai taikhan ke pathaise, bemar manu ke changai kori bole aru Isor rajyo laga kotha kobole nimite.
3 Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
Aru Jisu taikhan ke koise, “Eku loi najabi- tumi laga jola, lathi, poisa aru bhaat, duita kapra bhi loi najabi.
4 Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
Juntu ghor te ghusi bo, ta te he thakibi, jitia tak etu jaga to nachare.
5 Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
Jun jagate tumikhan ke namate, etu sheher pora ula homoi te, tumi laga theng pora dhuli to hatai dibi, etu he taikhan bhirodh te ekta sakhi hobo.”
6 Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
Aru taikhan alag hoi kene bosti khan phale jai jaise, Isor laga kotha prochar kori kene, sob jagate changai kori kene jaise.
7 Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
Jitia Herod raja pora etukhan sob hunise, tai bhoi hoi kene bhabona korise, kelemane kunba pora koise John to mora pora jinda hoise,
8 Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
aru kunba koise Elijah he ahise, aru kunba pora koise, poila laga bhabobadi ekjon jinda hoise.
9 Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
Kintu Herod koise, “Moi John laga matha alag kori dise, kintu etu kun ase jun laga moi iman kotha huni ase?” Aru tai Jisu ke sabole kosis kori thakise.
10 Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
Aru jitia apostle khan wapas ahise, taikhan ki korise etu sob Jisu ke koi dise. Titia Jisu pora taikhan ke loi jaise, aru ekdom chup-chap pora Bethsaida sheher te taikhan sob jai jaise.
11 Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
Kintu jitia manu laga bhir khan etu hunise, taikhan bhi Jisu piche korise. Titia Tai sobke matise aru Isor laga rajyo kotha taikhan logote koise, aru jun manu changai lage, taikhan ke changai korise.
12 Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
Etiya saam hobole homoi hoise, baroh jon chela khan Tai usorte ahikena koise, “Manu laga bhir khan ke pathai dibi, taikhan usor bosti te jai kene ghuma bole aru khabole bisaribo, kelemane moi khan eku napai-a jagate ase.”
13 Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
Kintu Jisu taikhan ke koise, “Tumikhan manu khan ke kiba khabole dibi.” Kintu taikhan koise, “Moi khan logote pasta roti aru duita maas he ase- jodi moi khan jai kene sob manu nimite khana kina nai koile.”
14 Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
-Ta te panch hajar manu thakise.- Titia Tai pora chela khan ke koise, “Taikhan ke ekta bhag te pachas manu kori kene bohibo dibi.”
15 Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
Aru taikhan eneka korise aru sobke bohi bole dise.
16 Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
Pasta roti aru duita maas to hathte loi kene, Tai sorgo phale saise, dhonyabad dise aru bhangaikena chela khan ke dibole dise.
17 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Taikhan sob khai kene bhorta hoise, aru bachi juwa sob uthaise- aru baroh ta tukri te uthaise.
18 Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
Aru ek din eneka hoise jitia Jisu Tai ekla pora prathana kori thakise, aru chela khan bhi Tai logote thakise, aru Tai taikhan ke hudise, “Manu khan pora Moi kun ase koi?”
19 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
Taikhan koise, “Baptizma Diya John Aru kunba koi Elijah, aru dusra khan pora koi purana homoi pora jinda huwa bhabobadi ekjon.”
20 Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
Titia Tai taikhan ke koise, “Kintu tumikhan Moi kun ase koi?” Titia Peter he koise, “Isor laga Khrista.”
21 Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
Kintu Tai pora taikhan ke etu kotha kunke bhi nokobole koise.
22 Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
Tai koise, “Manu laga Putro bisi dukh pabo aru cholawta khan Taike swekar nakoribo, mukhyo purohit khan aru niyom likha khan pora bhi golti dhoribo aru Taike morai dibo, kintu Tai tin dinte arubi jinda hobo.”
23 Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
Aru Tai sobke koise, “Kunba manu Moi pichete ahibole itcha thakile, tai nijorke pahoribo lage aru hodai cross uthaikene moi pichete ahibo lage.
24 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
Jun manu tai laga jibon to bacha bole kaam koribo tai harai dibo; kintu jun manu moi nimite jibon dibo, tai jibon pabo.
25 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
Jibon te ki labh ase, sob duniya to paile bhi, nijor jibon to nuksan korile?
26 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
Kun manu moi laga kotha aru moi nimite sorom kore, jitia Manu laga Putro Tai nijor laga mohima aru Baba laga mohima aru pobitro sorgodoth khan laga mohima pora wapas ahibo, etu homoi te etu manu nimite moi bhi sorom hobo.
27 Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
Kintu moi hosa kotha koi ase, kunba manu khan yate rukhi ase, taikhan Isor laga rajyo nadikha tak namoribo.”
28 Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
Etu kotha khan kowa ath din pichete, Tai tilla uporte prathana kori bole jaise, Peter, John aru James khan ke loi kene.
29 Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
Jitia Tai prathana kori thakise, Tai laga chehera bodli hoise, aru Tai laga kapra to asurit laga boga hoise.
30 Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
Aru sabi, duijon manu Tai logote kotha koi thakise, Moses aru Elijah thakise,
31 Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
Mohima pora taikhan ahise, tai jabo laga kotha to patise, juntu Jerusalem te pura hoi jabo.
32 Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
Jitia Peter aru sathi khan ghumai thakise, aru uthise, taikhan Tai laga mohima dikhise, aru duijon manu Tai logote khara hoi thaka dikhise.
33 Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
Pichete eneka hoise, jitia duijon manu Jisu usor pora jai thakise, Peter Taike koise, “Probhu, amikhan yate tinta khamba bonabo, ekta apuni nimite, ekta Moses karone, aru ekta Elijah karone.” -Tai ki koi thakise tai najane.-
34 Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
Kintu jitia tai etu koise, ekta badal ahikena taikhan ke lukai dise, aru taikhan bhoi lagise.
35 Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
Aru akas pora ekta awaj ahise, “Etu Ami laga Putro ase, junke Moi basi loise; Tai laga kotha huni bhi.”
36 Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
Jitia etu kotha khotom hoise, taikhan Jisu ekla thaka dikhise. Taikhan chup thakise aru ki dikhise kunke bhi kowa nai.
37 Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
Aru ek dinte eneka hoise, jitia taikhan pahar upor pora nichete ahise, dangor bhir ke lok paise.
38 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
Aru sabi, ekjon manu majot pora hala kori, koise, “Sikhai diya manu, moi anurodh korise, ami laga bacha ke sabi, tai moi laga ekjon bacha he ase.
39 Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
Sabi, ekjon atma achanak pora dhori kene tai laga mukh pora letera thuk ulaise. Aru taike jokhom kori kene ulai jaise.
40 Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
Moi Apuni laga chela khan ke atma kheda bole anurodh korise, kintu taikhan kheda bole para nai.”
41 Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
Titia Jisu taikhan ke jowab dise, “Biswas nathaka aru biya rasta te jai thaka manu khan, Moi tumikhan logote kiman din thakibo? Tumi laga chokra ke yate anibi.”
42 Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
Jitia chokra ke ani thakise, atma pora taike matite girai kene bisi hilai dise. Kintu Jisu pora dusto atma ke gali dise, aru chokra ke bhal kori dise, aru tai baba logot di dise.
43 Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
Taikhan Isor laga asurit kaam to dikhise. Kintu jitia manu khan ki hoise etu dikhise taikhan asurit lagise, Jisu tai laga chela khan ke koise,
44 “Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
“Etu kotha tumikhan mon bhitor te jabole dibi: kele koile Manu laga Putro ke manu laga hathte thogai pora di dibole ase.”
45 Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
Kintu taikhan etu kotha bujhi bole para nai. Etu kotha taikhan pora lukai kene thakise, etu karone taikhan bujhi bole para nai, aru taikhan Jisu ke etu kotha hudibole bhoi lagise.
46 Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
Pichete chela khan majote kun he sob pora dangor hobo itu laga kotha ulaise.
47 Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
Kintu Jisu taikhan laga monte ki bhabona kori ase etu jani loise, aru ekjon chutu bacha ke Tai usorte uthai loise,
48 Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
aru taikhan ke koise, “Jun manu etu bacha ke Moi laga naam pora grohon kore, tai Moike grohon kore; aru jun manu Moike grohon kore, jun Moike pathaise Taike bhi grohon kore. Kun manu nijorke chutu koribo, tai he dangor hobo.”
49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
John koise, “Probhu, amikhan dikhise kunba manu Apuni laga naam pora bhoot khedai se aru amikhan taike rukhai dise, kele koile tai moi khan logot nohoi.”
50 Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
Kintu Jisu pora taikhan ke koise, “Taikhan ke narukhabi, jun manu tumikhan bhirodh te nai, tai tumikhan logote ase.”
51 Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
Etiya, Taike sorgote uthai loi jabole laga din to usorte hoise, Tai Jerusalem te jabole bisi mon hoise.
52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
Tai poila ekjon chela ke pathaise, aru taikhan Samaria bosti bhitor te punchi kene sob kaam taiyar korise.
53 lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
Kintu ta te thaka manu khan Taike grohon kora nai, kelemane tai Jerusalem te jabole he mon thakise.
54 Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
Aru jitia chela khan James aru John ke dikhise, taikhan koise, “Probhu, amikhan sorgo pora jui ahi kene taikhan ke khotom kori bole kobo naki?”
55 Yesu akageuka na kuwakemea,
Kintu Tai ghuri kene taikhan ke gali dise,
56 nao wakaenda kijiji kingine.
aru taikhan ta te pora alag bosti te jaise.
57 Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
Taikhan rasta te jai thaka homoi te, kunba ekjon Jisu ke koise, “Apuni kun jagate jabo moi bhi apuni logote jabo.”
58 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
Jisu taike koise, “Siyal khan laga bhi gath ase aru akas te chiriya khan laga bhi ghor ase, hoile bhi Manu laga Putro laga matha rakhibole eku bhi jaga nai.”
59 Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
Titia Jisu aru ekjon ke koise, “Moi laga piche ahibi.” Kintu tai koise, “Probhu, poila moi jai kene moi laga baba ke kobor dikene ahibo.”
60 Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
Kintu Tai koise, “Mora khan pora mora khan ke kobor dibo. Kintu tumi, jai kene Isor laga rajyo prochar koribi.”
61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
Aru ekjon koise, “Moi bhi Apuni laga piche ahibo, Probhu, kintu moi poila jai kene sob ghor manu ke jai ase kobo.”
62 Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”
Kintu Jisu koise, “Jun manu kheti te hal dhori kene pichete nasai, tai he Isor laga rajyo nimite thik ase.”

< Luka 9 >