< Luka 4 >
1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
And Jesus, filled with the Holy Spirit, returned from the Jordan. And he was urged by the Spirit into the wilderness
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
for forty days, and he was tested by the devil. And he ate nothing in those days. And when they were completed, he was hungry.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
Then the devil said to him, “If you are the Son of God, speak to this stone, so that it may be made into bread.”
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
And Jesus answered him, “It is written: ‘Man shall not live by bread alone, but by every word of God.’”
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
And the devil led him onto a high mountain, and he showed him all the kingdoms of the world in a moment of time,
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
and he said to him: “To you, I will give all this power, and its glory. For they have been handed over to me, and I give them to whomever I wish.
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
Therefore, if you will worship before me, all will be yours.”
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
And in response, Jesus said to him: “It is written: ‘You shall worship the Lord your God, and you shall serve him alone.’”
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
And he brought him to Jerusalem, and he set him on the parapet of the temple, and he said to him: “If you are the Son of God, cast yourself down from here.
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
For it is written that he has given his Angels charge over you, so that they may guard you,
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and so that they may take you into their hands, lest perhaps you may hurt your foot against a stone.”
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
And in response, Jesus said to him, “It is said: ‘You shall not tempt the Lord your God.’”
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
And when all the temptation was completed, the devil withdrew from him, until a time.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
And Jesus returned, in the power of the Spirit, into Galilee. And his fame spread throughout the entire region.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
And he taught in their synagogues, and he was magnified by everyone.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
And he went to Nazareth, where he had been raised. And he entered into the synagogue, according to his custom, on the Sabbath day. And he rose up to read.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
And the book of the prophet Isaiah was handed to him. And as he unrolled the book, he found the place where it was written:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
“The Spirit of the Lord is upon me; because of this, he has anointed me. He has sent me to evangelize the poor, to heal the contrite of heart,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
to preach forgiveness to captives and sight to the blind, to release the broken into forgiveness, to preach the acceptable year of the Lord and the day of retribution.”
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
And when he had rolled up the book, he returned it to the minister, and he sat down. And the eyes of everyone in the synagogue were fixed on him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
Then he began to say to them, “On this day, this scripture has been fulfilled in your hearing.”
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
And everyone gave testimony to him. And they wondered at the words of grace that proceeded from his mouth. And they said, “Is this not the son of Joseph?”
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
And he said to them: “Certainly, you will recite to me this saying, ‘Physician, heal yourself.’ The many great things that we have heard were done in Capernaum, do here also in your own country.”
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
Then he said: “Amen I say to you, that no prophet is accepted in his own country.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
In truth, I say to you, there were many widows in the days of Elijah in Israel, when the heavens were closed for three years and six months, when a great famine had occurred throughout the entire land.
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
And to none of these was Elijah sent, except to Zarephath of Sidon, to a woman who was a widow.
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
And there were many lepers in Israel under the prophet Elisha. And none of these was cleansed, except Naaman the Syrian.”
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
And all those in the synagogue, upon hearing these things, were filled with anger.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
And they rose up and drove him beyond the city. And they brought him all the way to the edge of the mount, upon which their city had been built, so that they might throw him down violently.
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
But passing through their midst, he went away.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
And he descended to Capernaum, a city of Galilee. And there he taught them on the Sabbaths.
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
And they were astonished at his doctrine, for his word was spoken with authority.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
And in the synagogue, there was a man who had an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
saying: “Let us alone. What are we to you, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know you who you are: the Holy One of God.”
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
And Jesus rebuked him, saying, “Be silent and depart from him.” And when the demon had thrown him into their midst, he departed from him, and he no longer harmed him.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
And fear fell over them all. And they discussed this among themselves, saying: “What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits, and they depart.”
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
And his fame spread to every place in the region.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
Then Jesus, rising up from the synagogue, entered into the house of Simon. Now Simon’s mother-in-law was in the grip of a severe fever. And they petitioned him on her behalf.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
And standing over her, he commanded the fever, and it left her. And promptly rising up, she ministered to them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
Then, when the sun had set, all those who had anyone afflicted with various diseases brought them to him. Then, laying his hands on each one of them, he cured them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
Now demons departed from many of them, crying out and saying, “You are the son of God.” And rebuking them, he would not permit them to speak. For they knew him to be the Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
Then, when it was daytime, going out, he went to a deserted place. And the crowds sought him, and they went all the way to him. And they detained him, so that he would not depart from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
And he said to them, “I must also preach the kingdom of God to other cities, because it was for this reason that I was sent.”
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
And he was preaching in the synagogues of Galilee.