< Yohana 1 >
1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
In the beginning was the Word, and the Word was with God, and God was the Word.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
He was with God in the beginning.
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
All things were made through Him, and nothing that was made was made without Him.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
Life was in Him, and Life was the light of men.
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
And the light shines in the darkness, and the darkness did not comprehend it.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
There was a man sent by God, whose name was John.
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
He arrived as a witness to offer testimony about the Light, so that all would believe through him.
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
He was not the Light, but he was to offer testimony about the Light.
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
The true Light, which illuminates every man, was coming into this world.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
He was in the world, and the world was made through him, and the world did not recognize him.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
He went to his own, and his own did not accept him.
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
Yet whoever did accept him, those who believed in his name, he gave them the power to become the sons of God.
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
These are born, not of blood, nor of the will of flesh, nor of the will of man, but of God.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
And the Word became flesh, and he lived among us, and we saw his glory, glory like that of an only-begotten Son from the Father, full of grace and truth.
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
John offers testimony about him, and he cries out, saying: “This is the one about whom I said: ‘He who is to come after me, has been placed ahead of me, because he existed before me.’”
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
And from his fullness, we all have received, even grace for grace.
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
For the law was given through Moses, but grace and truth came through Jesus Christ.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
No one ever saw God; the only-begotten Son, who is in the bosom of the Father, he himself has described him.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
And this is the testimony of John, when the Jews sent priests and Levites from Jerusalem to him, so that they might ask him, “Who are you?”
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
And he confessed it and did not deny it; and what he confessed was: “I am not the Christ.”
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
And they questioned him: “Then what are you? Are you Elijah?” And he said, “I am not.” “Are you the Prophet?” And he answered, “No.”
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
Therefore, they said to him: “Who are you, so that we may give an answer to those who sent us? What do you say about yourself?”
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
He said, “I am a voice crying out in the desert, ‘Make straight the way of the Lord,’ just as the prophet Isaiah said.”
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
And some of those who had been sent were from among the Pharisees.
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
And they questioned him and said to him, “Then why do you baptize, if you are not the Christ, and not Elijah, and not the Prophet?”
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
John answered them by saying: “I baptize with water. But in your midst stands one, whom you do not know.
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
The same is he who is to come after me, who has been placed ahead of me, the laces of whose shoes I am not worthy to loosen.”
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
These things happened in Bethania, across the Jordan, where John was baptizing.
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
On the next day, John saw Jesus coming toward him, and so he said: “Behold, the Lamb of God. Behold, he who takes away the sin of the world.
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
This is the one about whom I said, ‘After me arrives a man, who has been placed ahead of me, because he existed before me.’
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
And I did not know him. Yet it is for this reason that I come baptizing with water: so that he may be made manifest in Israel.”
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
And John offered testimony, saying: “For I saw the Spirit descending from heaven like a dove; and he remained upon him.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
And I did not know him. But he who sent me to baptize with water said to me: ‘He over whom you will see the Spirit descending and remaining upon him, this is the one who baptizes with the Holy Spirit.’
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
And I saw, and I gave testimony: that this one is the Son of God.”
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
The next day again, John was standing with two of his disciples.
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
And catching sight of Jesus walking, he said, “Behold, the Lamb of God.”
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
And two disciples were listening to him speaking. And they followed Jesus.
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
Then Jesus, turning around and seeing them following him, said to them, “What are you seeking?” And they said to him, “Rabbi (which means in translation, Teacher), where do you live?”
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
He said to them, “Come and see.” They went and saw where he was staying, and they stayed with him that day. Now it was about the tenth hour.
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
And Andrew, the brother of Simon Peter, was one of the two who had heard about him from John and had followed him.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
First, he found his brother Simon, and he said to him, “We have found the Messiah,” (which is translated as the Christ).
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
And he led him to Jesus. And Jesus, gazing at him, said: “You are Simon, son of Jonah. You shall be called Cephas,” (which is translated as Peter).
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
On the next day, he wanted to go into Galilee, and he found Philip. And Jesus said to him, “Follow me.”
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
Now Philip was from Bethsaida, the city of Andrew and Peter.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Philip found Nathanael, and he said to him, “We have found the one about whom Moses wrote in the Law and the Prophets: Jesus, the son of Joseph, from Nazareth.”
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
And Nathanael said to him, “Can anything good be from Nazareth?” Philip said to him, “Come and see.”
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
Jesus saw Nathanael coming toward him, and he said about him, “Behold, an Israelite in whom truly there is no deceit.”
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
Nathanael said to him, “From where do you know me?” Jesus responded and said to him, “Before Philip called you, when you were under the fig tree, I saw you.”
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
Nathanael answered him and said: “Rabbi, you are the Son of God. You are the King of Israel.”
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
Jesus responded and said to him: “Because I told you that I saw you under the fig tree, you believe. Greater things than these, you will see.”
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
And he said to him, “Amen, amen, I say to you, you will see heaven opened, and the Angels of God ascending and descending over the Son of man.”