< Luka 21 >
1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Il leva les yeux et vit les riches qui mettaient leurs dons dans le trésor.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
Il vit une pauvre veuve qui jetait deux petites pièces d'airain.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
Il dit: « Je vous le dis en vérité, cette pauvre veuve a mis plus qu'eux tous,
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
car tous ceux-là ont fait des dons à Dieu de leur superflu, mais elle, de sa pauvreté, a mis tout ce qu'elle avait pour vivre. »
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
Comme certains parlaient du temple et de la façon dont il était décoré de belles pierres et de cadeaux, il dit:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
« Quant à ces choses que vous voyez, les jours viendront où il ne restera pas ici une pierre sur une autre qui ne soit pas renversée. »
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
Ils lui demandèrent: « Maître, quand donc ces choses arriveront-elles? Quel est le signe que ces choses vont arriver? »
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
Il dit: « Prenez garde de ne pas vous laisser égarer, car plusieurs viendront en mon nom, disant: « C'est moi", et « Le temps est proche ». Ne les suivez donc pas.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
Quand vous entendrez parler de guerres et de troubles, ne soyez pas terrifiés, car il faut que ces choses arrivent d'abord, mais la fin ne viendra pas immédiatement. »
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Puis il leur dit: « Une nation s'élèvera contre une nation, et un royaume contre un royaume.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
Il y aura de grands tremblements de terre, des famines et des pestes en divers lieux. Il y aura des terreurs et de grands signes venant du ciel.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
Mais avant tout cela, on mettra la main sur vous, on vous persécutera, on vous livrera aux synagogues et aux prisons, on vous fera comparaître devant des rois et des gouverneurs, à cause de mon nom.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
Il en résultera pour vous un témoignage.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Mettez-vous donc dans la tête de ne pas réfléchir d'avance à la manière de répondre,
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
car je vous donnerai une bouche et une sagesse auxquelles tous vos adversaires ne pourront résister ni contredire.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
Vous serez livrés même par vos parents, vos frères, vos proches et vos amis. Ils feront mettre à mort certains d'entre vous.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
Vous serez haïs de tous les hommes à cause de mon nom.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
Et pas un cheveu de votre tête ne périra.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
« C'est par votre endurance que vous gagnerez vos vies.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
« Mais quand vous verrez Jérusalem entourée d'armées, sachez que sa désolation est proche.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Alors, que ceux qui sont en Judée fuient vers les montagnes. Que ceux qui sont au milieu d'elle s'en aillent. Que ceux qui sont dans la campagne n'y entrent pas.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
Car ce sont des jours de vengeance, afin que s'accomplisse tout ce qui est écrit.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Malheur aux femmes enceintes et à celles qui allaitent en ces jours-là! Car il y aura une grande détresse dans le pays et une grande colère pour ce peuple.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
Ils tomberont sous le tranchant de l'épée, et ils seront emmenés captifs dans toutes les nations. Jérusalem sera foulée aux pieds par les païens, jusqu'à ce que les temps des païens soient accomplis.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
Il y aura des signes dans le soleil, la lune et les étoiles; et sur la terre, l'angoisse des nations, dans la perplexité à cause du mugissement de la mer et des flots;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
les hommes seront saisis de crainte et d'attente des choses qui vont arriver au monde, car les puissances des cieux seront ébranlées.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
Alors ils verront le Fils de l'homme venant sur une nuée avec puissance et grande gloire.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
Mais quand ces choses commenceront à arriver, regardez en haut et levez vos têtes, car votre rédemption est proche. »
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
Il leur raconta une parabole. « Regardez le figuier et tous les arbres.
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
Quand ils bourgeonnent déjà, vous le voyez et vous savez par vous-mêmes que l'été est déjà proche.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
De même, vous aussi, quand vous voyez ces choses arriver, vous savez que le Royaume de Dieu est proche.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera pas que tout ne soit accompli.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront pas.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
« Prenez donc garde que vos cœurs ne s'appesantissent sous le poids des plaisirs de la fête, de l'ivresse et des soucis de la vie présente, et que ce jour ne vienne sur vous à l'improviste.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
Car il viendra comme un piège pour tous ceux qui habitent à la surface de toute la terre.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Veillez donc en permanence, en priant pour que vous soyez jugés dignes d'échapper à toutes ces choses qui arriveront, et de vous présenter devant le Fils de l'homme. »
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
Chaque jour, Jésus enseignait dans le temple, et chaque soir, il sortait et passait la nuit sur la montagne qu'on appelle le mont Olivet.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
Tout le peuple venait de bon matin le trouver dans le temple pour l'écouter.