< Marko 1 >

1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Le début de la Bonne Nouvelle de Jésus-Christ, le Fils de Dieu.
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
Comme il est écrit dans les prophètes, « Voici que j'envoie mon messager devant ta face, qui préparera ton chemin devant toi:
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
la voix de celui qui crie dans le désert, Préparez le chemin du Seigneur! Rends ses chemins droits! »
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
Jean vint baptiser dans le désert et prêcher le baptême de repentance pour le pardon des péchés.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
Tout le pays de Judée et tous ceux de Jérusalem se rendirent auprès de lui. Ils se faisaient baptiser par lui dans le Jourdain, en confessant leurs péchés.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
Jean était vêtu de poils de chameau et portait une ceinture de cuir à la taille. Il se nourrissait de sauterelles et de miel sauvage.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
Il prêchait, disant: « Après moi vient celui qui est plus puissant que moi, et dont je ne suis pas digne de délier la lanière de ses sandales.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
Je vous ai baptisés dans l'eau, mais lui vous baptisera dans l'Esprit Saint. »
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
En ce temps-là, Jésus vint de Nazareth, en Galilée, et fut baptisé par Jean dans le Jourdain.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
Aussitôt remonté de l'eau, il vit les cieux se fendre et l'Esprit descendre sur lui comme une colombe.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
Une voix sortit du ciel: « Tu es mon Fils bien-aimé, en qui j'ai mis toute mon affection. »
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
Aussitôt, l'Esprit le poussa dans le désert.
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
Il resta là, dans le désert, quarante jours, tenté par Satan. Il était avec les animaux sauvages, et les anges le servaient.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
Après que Jean eut été mis en détention, Jésus vint en Galilée, prêchant la Bonne Nouvelle du Royaume de Dieu,
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
et disant: « Le temps est accompli, et le Royaume de Dieu est tout proche. Repentez-vous, et croyez à la Bonne Nouvelle. »
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
En passant le long de la mer de Galilée, il vit Simon et André, le frère de Simon, qui jetaient un filet dans la mer, car ils étaient pêcheurs.
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
Jésus leur dit: « Venez après moi, et je ferai de vous des pêcheurs d'hommes. »
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
Aussitôt, ils laissèrent leurs filets et le suivirent.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
S'éloignant un peu de là, il vit Jacques, fils de Zébédée, et Jean, son frère, qui étaient aussi dans la barque pour réparer les filets.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
Aussitôt, il les appela, et ils laissèrent leur père Zébédée dans la barque avec les mercenaires, et le suivirent.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
Ils se rendirent à Capernaüm, et aussitôt, le jour du sabbat, il entra dans la synagogue et enseigna.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
Ils étaient étonnés de son enseignement, car il les enseignait comme ayant autorité, et non comme les scribes.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
Aussitôt, il se trouva dans leur synagogue un homme possédé d'un esprit impur, qui poussa un cri
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
en disant: « Ah! qu'avons-nous à faire avec toi, Jésus, Nazaréen? Es-tu venu pour nous détruire? Je sais qui tu es: le Saint de Dieu! »
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
Jésus le réprimanda en disant: « Tais-toi, et sors de lui! »
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
L'esprit impur, qui le convulsait et criait d'une voix forte, sortit de lui.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
Tous étaient stupéfaits, et ils s'interrogeaient entre eux, disant: Qu'est-ce que cela? Une nouvelle doctrine? Car il commande avec autorité même aux esprits impurs, et ils lui obéissent! »
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
La nouvelle de sa venue se répandit aussitôt partout dans toute la région de la Galilée et ses environs.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
Aussitôt sortis de la synagogue, ils entrèrent dans la maison de Simon et d'André, avec Jacques et Jean.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
Or, la mère de la femme de Simon était malade de la fièvre, et aussitôt on lui en parla.
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
Il vint, la prit par la main et la fit lever. La fièvre la quitta aussitôt, et elle les servit.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
Le soir, au coucher du soleil, on lui amena tous les malades et ceux qui étaient possédés par des démons.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
Toute la ville était rassemblée à la porte.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
Il guérit beaucoup de malades atteints de diverses maladies et chassa beaucoup de démons. Il ne permettait pas aux démons de parler, car ils le connaissaient.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
De bon matin, comme il faisait encore nuit, il se leva et sortit, et s'en alla dans un lieu désert, où il pria.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
Simon et ceux qui étaient avec lui le cherchaient.
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
Ils le trouvèrent et lui dirent: « Tout le monde te cherche. »
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
Il leur dit: « Allons ailleurs, dans les villes voisines, afin que j'y prêche aussi, car c'est pour cela que je suis sorti. »
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
Il allait dans leurs synagogues, dans toute la Galilée, prêchant et chassant les démons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
Un lépreux s'approcha de lui, le supplia, se mit à genoux devant lui et lui dit: « Si tu le veux, tu peux me rendre pur. »
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
Ému de compassion, il étendit sa main, le toucha et lui dit: « Je le veux. Sois purifié. »
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
Dès qu'il eut dit cela, la lèpre se retira aussitôt de lui et il fut rendu pur.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
Il lui donna un avertissement strict et le renvoya aussitôt,
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
en lui disant: « Veille à ne rien dire à personne, mais va te montrer au prêtre et offre pour ta purification les choses que Moïse a prescrites, en témoignage pour eux. »
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
Mais il sortit, et se mit à faire beaucoup de publicité, et à répandre l'affaire, de sorte que Jésus ne pouvait plus entrer ouvertement dans une ville, mais se tenait dehors, dans des lieux déserts. Les gens venaient à lui de partout.

< Marko 1 >