< Mambo ya Walawi 3 >

1 “‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
«هرگاه کسی بخواهد قربانی سلامتی به خداوند تقدیم کند، می‌تواند برای این کار از گاو نر یا ماده استفاده نماید. حیوانی که به خداوند تقدیم می‌شود باید سالم و بی‌عیب باشد.
2 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
شخصی که حیوان را تقدیم می‌کند، باید دست خود را روی سر آن بگذارد و دم در خیمۀ ملاقات سرش را ببرد. پسران هارون خون آن را بر چهار طرف مذبح بپاشند.
3 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
کاهن باید بخشی از این قربانی سلامتی را به عنوان هدیۀ اختصاصی به خداوند تقدیم کند. این هدیه شامل چربی داخل شکم،
4 figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
دو قلوه و چربی روی آنها در قسمت تهیگاه و سفیدی روی جگر خواهد بود. اینها باید همراه قلوه‌ها خارج شوند،
5 Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
و پسران هارون آنها را بر مذبح، روی قربانی سوختنی، بسوزانند. این هدیه، هدیه‌ای مخصوص و خوشبو برای خداوند است.
6 “‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
«برای قربانی سلامتی می‌توان گوسفند و بز (نر یا ماده) که سالم و بی‌عیب باشند نیز به خداوند تقدیم کرد.
7 Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
اگر قربانی، گوسفند باشد، شخصی که آن را به خداوند تقدیم می‌کند باید آن را به حضور خداوند آورده،
8 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
دستش را روی سر حیوان بگذارد و دم در خیمۀ ملاقات سرش را ببرد. سپس پسران هارون خون آن را بر چهار طرف مذبح بپاشند.
9 Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
کاهن باید چربی این قربانی سلامتی را به عنوان هدیۀ مخصوص به خداوند تقدیم کند. این چربی شامل دنبه که از نزدیکی ستون مهره‌ها جدا شده، و تمام چربی داخل شکم،
10 figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
دو قلوه و چربی روی آنها در قسمت تهیگاه، و سفیدی روی جگر می‌باشد. اینها همراه با قلوه‌ها باید جدا شوند
11 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
و کاهن آنها را همچون هدیۀ مخصوص خوراکی به خداوند تقدیم کرده، بر آتش مذبح بسوزاند.
12 “‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
«اگر قربانی، بز باشد، شخصی که آن را به خداوند تقدیم می‌کند، باید آن را به حضور خداوند آورده،
13 Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
دستش را روی سر حیوان بگذارد و دم در خیمۀ ملاقات سرش را ببرد. سپس پسران هارون خون آن را بر چهار طرف مذبح بپاشند
14 Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
کاهن باید قسمتی از این قربانی را به عنوان هدیۀ مخصوص به خداوند تقدیم کند. این شامل چربی داخل شکم،
15 figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
و قلوه و چربی روی آنها در قسمت تهیگاه، و سفیدی روی جگر می‌باشد. اینها همراه با قلوه‌ها باید جدا شوند.
16 Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
سپس کاهن این همه را به عنوان خوراک بر مذبح بسوزاند. این هدیه، هدیه‌ای مخصوص و خوشبو برای خداوند است. تمام چربی آن حیوان به خداوند تعلق دارد.
17 “‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”
هیچ‌یک از شما نباید خون یا چربی بخورید. این قانونی است ابدی برای شما و نسلهایتان، در هر جا که باشید.»

< Mambo ya Walawi 3 >