< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
Pakomuta! Fuka mukela lun Jerusalem, su sie pacl ah sessesla ke mwet. Sie pacl ah akfulatyeyuk el sin faclu nufon, a inge el supwar oana sie katinmas. Meet el arulana fulat, a inge el putatyang nu in moul in mwet kohs.
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
El tung ke fong nufon, ac sroninmutal sorori ke likintupal. Inmasrlon mwet kawuk lal meet ah nufon, tiana sie lula in akwoyal. Mwet asruoki nu sel meet ah sisella, ac inge elos nukewa lainul.
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
Mwet Judah elos mwet kohs ke sripen lillilyak elos liki acn selos. Elos muta in facl saya, ac wangin acn elos in pangon acn selos sifacna. Mwet lokoalok lalos raunelosla, ac wangin innek in kaingla lalos.
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
Wanginla mwet tuku nu ke Tempul in pacl inge in tuh alu ke len mutal. Tulik mutan su tuh alullul we elos muta in keok, ac mwet tol elos sasao na. Mutunpot in siti uh oalallana, ac acn Zion oan in ongoiya lulap.
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
Mwet lokoalok lal elos kutangulla, ac el oan ye ku lalos. LEUM GOD El oru elan keok ke sripen ma koluk puspis lal. Tulik natul uh sruoh ac utukla lukel.
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
Wolana lun Jerusalem wanginla, Mwet kol lalos elos oana deer ma munasla ke masrinsral, Su apkuran in wanginla ku la ke elos kaingkin mwet ma ukwalos uh.
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
Ke Jerusalem el musalla ac mukaimtalla in pacl inge, el esamak ma nukewa ma wo nu sel meet ah. Ke el putatyang nu inpoun mwet lokoalok lal, wangin sie acn ku in kasrel mweuni mwet lokoalok lal. Mwet kutangulla uh isrunul ke el ikori.
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
Wanginla sunakinyal; el koflufolla, ac sununteiyuk el. El sao ac wikin mutal ke mwekin. Jerusalem el aktaekyal sifacna ke ma koluk lulap lal.
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
Ma fohkfok lal arulana mohtotla, tusruktu wanginna nunkeyen ma ac sikyak uh sel. Ikori lal ah arulana koluk, ac wangin sie mwet ku in akwoyal. Mwet lokoalok lal elos kutangla, ac el wowoyak nu sin LEUM GOD ac siyuk ke pakoten lal.
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
Mwet lokoalok lal elos pisrala ma saok lal nukewa. El sifacna liye ke elos utyak nu in Tempul, Yen LEUM GOD El tia lela mwet pegan in utyak nu we.
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
Mwet lal elos sasao ke sukyen ma elos in kang; Elos sang ma saok lalos ayaol mwe mongo in sruokya moul lalos. Ac siti uh wowoyak ac fahk, “Liyeyu, LEUM GOD. Liyeyu in keok luk.”
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
El pang nu selos nukewa su fufahsryesr yen el muta we, ac fahk, “Ngetma liyeyu! Wangin sie mwet nu pulakin waiok oana nga, Waiok su ma LEUM GOD El use nu fuk in pacl in kasrkusrak lal.
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
“El supwama e lucng me, sie e su firirrir in nga. El filiya sie kwasrip nu sik ac sisyuwi nu infohk uh. Na El sisyula ac likiyuwi in mutana in waiok luk.
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
“El tuni ma koluk luk nukewa ac kapsreni nu sie; El sripisrya ke kwawuk, ac nga munasla ke toasriya uh. Leum El eisyuyang nu sin mwet lokoalok luk, ac wangin ma nga ku in oru in lainulos.
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
“Leum El isrun mwet mweun fokoko luk nukewa; El supwama sie un mwet mweun in tuh kunausla mwet fusr luk. El itungya mwet luk oana grape ke nien fut wain.
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
“Pa inge sripa se oru sroninmutuk kahkkakla uh. Wangin mwet ku in akwoyeyula; wangin mwet ku in akkeyeyu. Mwet lokoalok luk kutangyula; wangin kutena ma lula lun mwet luk.
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
“Nga asroela pouk, tuh wangin mwet in kasreyu. LEUM GOD El pangon mwet lokoalok liki acn nukewa in lainyu. Elos oreyu oana sie ma na olafohkfok.
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
“Tusruktu suwohs ma LEUM GOD El oru, mweyen nga tuh tia aksol. Porongeyu, kowos mwet yen nukewa; ngetma liyeyu in waiok luk. Mukul fusr ac mutan fusr luk elos utukla nu in sruoh.
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
“Nga pang nu sin mwet ma asruoki nu sik, tuh elos srunga kasreyu. Mwet tol ac mwet kol elos misa fin inkanek in siti uh Ke elos sukok mongo in sruokya moul lalos sifacna.
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
“O LEUM GOD, ngetma liye keok lulap lun ngunik! Insiuk arulana musalla ke asroeyen ma koluk luk. Oasr akmas orek ke inkanek uh; finne in lohm uh oasr pac misa.
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
“Porongo sasao luk; wanginna mwet in akwoyeyu. Mwet lokoalok luk elos engan lah kom ase ongoiya nu sik. Tari supwama len se ma kom tuh wulema kac ah; oru mwet lokoalok luk in keok oapana nga.
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
“Sang mwatalos ke ma koluk lalos nukewa. Kalyaelos oana ke kom tuh kalyeiyu ke ma koluk luk. Nga sasao in keok luk, ac insiuk musallana.”

< Maombolezo 1 >