< Yoshua 9 >

1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
and to be like/as to hear: hear all [the] king which in/on/with side: beyond [the] Jordan in/on/with mountain: mount and in/on/with Shephelah and in/on/with all coast [the] sea [the] Great (Sea) to(wards) opposite [the] Lebanon [the] Hittite and [the] Amorite [the] Canaanite [the] Perizzite [the] Hivite and [the] Jebusite
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
and to gather together to/for to fight with Joshua and with Israel lip one
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
and to dwell Gibeon to hear: hear [obj] which to make: do Joshua to/for Jericho and to/for Ai
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
and to make: do also they(masc.) in/on/with craftiness and to go: went and to take provision and to take: take sackcloth old to/for donkey their and wineskin wine old and to break up/open and to constrain
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
and sandal old and to spot in/on/with foot their and garment old upon them and all food: bread food their to wither to be crumb
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
and to go: went to(wards) Joshua to(wards) [the] camp [the] Gilgal and to say to(wards) him and to(wards) man Israel from land: country/planet distant to come (in): come and now to cut: make(covenant) to/for us covenant
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
(and to say *Q(K)*) man Israel to(wards) [the] Hivite perhaps in/on/with entrails: among my you(m. s.) to dwell and how? (to cut: make(covenant) *Q(k)*) to/for you covenant
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
and to say to(wards) Joshua servant/slave your we and to say to(wards) them Joshua who? you(m. p.) and from where? to come (in): come
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
and to say to(wards) him from land: country/planet distant much to come (in): come servant/slave your to/for name LORD God your for to hear: hear report his and [obj] all which to make: do in/on/with Egypt
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
and [obj] all which to make: do to/for two king [the] Amorite which in/on/with side: beyond [the] Jordan to/for Sihon king Heshbon and to/for Og king [the] Bashan which in/on/with Ashtaroth
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
and to say to(wards) us old: elder our and all to dwell land: country/planet our to/for to say to take: take in/on/with hand your provision to/for way: journey and to go: went to/for to encounter: meet them and to say to(wards) them servant/slave your we and now to cut: make(covenant) to/for us covenant
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
this food: bread our hot to provision [obj] him from house: home our in/on/with day to come out: come we to/for to go: come to(wards) you and now behold to wither and to be crumb
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
and these wineskin [the] wine which to fill new and behold to break up/open and these garment our and sandal our to become old from abundance [the] way: journey much
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
and to take: take [the] human from food their and [obj] lip: word LORD not to ask
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
and to make to/for them Joshua peace and to cut: make(covenant) to/for them covenant to/for to live them and to swear to/for them leader [the] congregation
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
and to be from end three day after which to cut: make(covenant) to/for them covenant and to hear: hear for near they(masc.) to(wards) him and in/on/with entrails: among his they(masc.) to dwell
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
and to set out son: descendant/people Israel and to come (in): come to(wards) city their in/on/with day [the] third and city their Gibeon and [the] Chephirah and Beeroth and Kiriath-jearim Kiriath-jearim
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
and not to smite them son: descendant/people Israel for to swear to/for them leader [the] congregation in/on/with LORD God Israel and to grumble all [the] congregation upon [the] leader
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
and to say all [the] leader to(wards) all [the] congregation we to swear to/for them in/on/with LORD God Israel and now not be able to/for to touch in/on/with them
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
this to make: do to/for them and to live [obj] them and not to be upon us wrath upon [the] oath which to swear to/for them
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
and to say to(wards) them [the] leader to live and to be to chop tree: wood and to draw water to/for all [the] congregation like/as as which to speak: speak to/for them [the] leader
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
and to call: call to to/for them Joshua and to speak: speak to(wards) them to/for to say to/for what? to deceive [obj] us to/for to say distant we from you much and you(m. p.) in/on/with entrails: among our to dwell
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
and now to curse you(m. p.) and not to cut: cut from you servant/slave and to chop tree: wood and to draw water to/for house: temple God my
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
and to answer [obj] Joshua and to say for to tell to tell to/for servant/slave your [obj] which to command LORD God your [obj] Moses servant/slave his to/for to give: give to/for you [obj] all [the] land: country/planet and to/for to destroy [obj] all to dwell [the] land: country/planet from face: before your and to fear much to/for soul: life our from face: because your and to make: do [obj] [the] word: thing [the] this
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
and now look! we in/on/with hand: power your like/as pleasant and like/as upright in/on/with eye: seeing your to/for to make: do to/for us to make: do
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
and to make: do to/for them so and to rescue [obj] them from hand: power son: descendant/people Israel and not to kill them
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
and to give: make them Joshua in/on/with day: today [the] he/she/it to chop tree: wood and to draw water to/for congregation and to/for altar LORD till [the] day: today [the] this to(wards) [the] place which to choose

< Yoshua 9 >