< Yoshua 10 >

1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
and to be like/as to hear: hear Adoni-zedek Adoni-zedek king Jerusalem for to capture Joshua [obj] [the] Ai and to devote/destroy her like/as as which to make: do to/for Jericho and to/for king her so to make: do to/for Ai and to/for king her and for to ally to dwell Gibeon with Israel and to be in/on/with entrails: among their
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
and to fear much for city great: large Gibeon like/as one city [the] kingdom and for he/she/it great: large from [the] Ai and all human her mighty man
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
and to send: depart Adoni-zedek Adoni-zedek king Jerusalem to(wards) Hoham king Hebron and to(wards) Piram king Jarmuth and to(wards) Japhia king Lachish and to(wards) Debir king Eglon to/for to say
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
to ascend: rise to(wards) me and to help me and to smite [obj] Gibeon for to ally with Joshua and with son: descendant/people Israel
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
and to gather and to ascend: rise five king [the] Amorite king Jerusalem king Hebron king Jarmuth king Lachish king Eglon they(masc.) and all camp their and to camp upon Gibeon and to fight upon her
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
and to send: depart human Gibeon to(wards) Joshua to(wards) [the] camp [the] Gilgal [to] to/for to say not to slacken hand your from servant/slave your to ascend: rise to(wards) us haste and to save [emph?] to/for us and to help us for to gather to(wards) us all king [the] Amorite to dwell [the] mountain: hill country
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
and to ascend: rise Joshua from [the] Gilgal he/she/it and all people [the] battle with him and all mighty man [the] strength
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
and to say LORD to(wards) Joshua not to fear from them for in/on/with hand: power your to give: give them not to stand: stand man: anyone from them in/on/with face: before your
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
and to come (in): come to(wards) them Joshua suddenly all [the] night to ascend: rise from [the] Gilgal
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
and to confuse them LORD to/for face: before Israel and to smite them wound great: large in/on/with Gibeon and to pursue them way: road ascent Beth-horon Beth-horon and to smite them till Azekah and till Makkedah
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
and to be in/on/with to flee they from face: before Israel they(masc.) in/on/with descent Beth-horon Beth-horon and LORD to throw upon them stone great: large from [the] heaven till Azekah and to die many which to die in/on/with stone [the] hail from whence to kill son: descendant/people Israel in/on/with sword
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
then to speak: speak Joshua to/for LORD in/on/with day to give: give LORD [obj] [the] Amorite to/for face: before son: descendant/people Israel and to say to/for eye: seeing Israel sun in/on/with Gibeon to silence: stationary and moon in/on/with valley Aijalon
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
and to silence: stationary [the] sun and moon to stand: stand till to avenge nation enemy his not he/she/it to write upon scroll: book [the] Jashar and to stand: stand [the] sun in/on/with half [the] heaven and not to hasten to/for to come (in): (sun)set like/as day unblemished: complete
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
and not to be like/as day [the] he/she/it to/for face: before his and after him to/for to hear: hear LORD in/on/with voice man for LORD to fight to/for Israel
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
and to return: return Joshua and all Israel with him to(wards) [the] camp [the] Gilgal [to]
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
and to flee five [the] king [the] these and to hide in/on/with cave in/on/with Makkedah
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
and to tell to/for Joshua to/for to say to find five [the] king to hide in/on/with cave in/on/with Makkedah
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
and to say Joshua to roll stone great: large to(wards) lip [the] cave and to reckon: overseer upon her human to/for to keep: guard them
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
and you(m. p.) not to stand: stand to pursue after enemy your and to cut off the tail [obj] them not to give: allow them to/for to come (in): come to(wards) city their for to give: give them LORD God your in/on/with hand: power your
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
and to be like/as to end: finish Joshua and son: descendant/people Israel to/for to smite them wound great: large much till to finish they and [the] survivor to escape from them and to come (in): come to(wards) city [the] fortification
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
and to return: return all [the] people to(wards) [the] camp to(wards) Joshua Makkedah in/on/with peace: well-being not to decide to/for son: descendant/people Israel to/for man: anyone [obj] tongue his
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
and to say Joshua to open [obj] lip [the] cave and to come out: send to(wards) me [obj] five [the] king [the] these from [the] cave
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
and to make: do so and to come out: send to(wards) him [obj] five [the] king [the] these from [the] cave [obj] king Jerusalem [obj] king Hebron [obj] king Jarmuth [obj] king Lachish [obj] king Eglon
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
and to be like/as to come out: send they [obj] [the] king [the] these to(wards) Joshua and to call: call to Joshua to(wards) all man Israel and to say to(wards) chief human [the] battle [the] to go: went with him to present: come to set: put [obj] foot your upon neck [the] king [the] these and to present: come and to set: put [obj] foot their upon neck their
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
and to say to(wards) them Joshua not to fear and not to to be dismayed to strengthen: strengthen and to strengthen for thus to make: do LORD to/for all enemy your which you(m. p.) to fight [obj] them
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
and to smite them Joshua after so and to die them and to hang them upon five tree and to be to hang upon [the] tree till [the] evening
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
and to be to/for time to come (in): (sun)set [the] sun to command Joshua and to go down them from upon [the] tree and to throw them to(wards) [the] cave which to hide there and to set: make stone great: large upon lip [the] cave till bone: same [the] day [the] this
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
and [obj] Makkedah to capture Joshua in/on/with day [the] he/she/it and to smite her to/for lip: edge sword and [obj] king her to devote/destroy [obj] them and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her not to remain survivor and to make: do to/for king Makkedah like/as as which to make: do to/for king Jericho
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
and to pass Joshua and all Israel with him from Makkedah Libnah and to fight with Libnah
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
and to give: give LORD also [obj] her in/on/with hand: power Israel and [obj] king her and to smite her to/for lip: edge sword and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her not to remain in/on/with her survivor and to make: do to/for king her like/as as which to make: do to/for king Jericho
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
and to pass Joshua and all Israel with him from Libnah Lachish [to] and to camp upon her and to fight in/on/with her
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
and to give: give LORD [obj] Lachish in/on/with hand: power Israel and to capture her in/on/with day [the] second and to smite her to/for lip: edge sword and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her like/as all which to make: do to/for Libnah
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
then to ascend: rise Horam king Gezer to/for to help [obj] Lachish and to smite him Joshua and [obj] people his till lest to remain to/for him survivor
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
and to pass Joshua and all Israel with him from Lachish Eglon [to] and to camp upon her and to fight upon her
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
and to capture her in/on/with day [the] he/she/it and to smite her to/for lip: edge sword and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her in/on/with day [the] he/she/it to devote/destroy like/as all which to make: do to/for Lachish
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
and to ascend: rise Joshua and all Israel with him from Eglon [to] Hebron [to] and to fight upon her
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
and to capture her and to smite her to/for lip: edge sword and [obj] king her and [obj] all city her and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her not to remain survivor like/as all which to make: do to/for Eglon and to devote/destroy [obj] her and [obj] all [the] soul: person which in/on/with her
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
and to return: return Joshua and all Israel with him Debir [to] and to fight upon her
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
and to capture her and [obj] king her and [obj] all city her and to smite them to/for lip: edge sword and to devote/destroy [obj] all soul: person which in/on/with her not to remain survivor like/as as which to make: do to/for Hebron so to make: do to/for Debir [to] and to/for king her and like/as as which to make: do to/for Libnah and to/for king her
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
and to smite Joshua [obj] all [the] land: country/planet [the] mountain: hill country and [the] Negeb and [the] Shephelah and [the] slope and [obj] all king their not to remain survivor and [obj] all [the] breath to devote/destroy like/as as which to command LORD God Israel
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
and to smite them Joshua from Kadesh-barnea Kadesh-barnea and till Gaza and [obj] all land: country/planet Goshen and till Gibeon
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
and [obj] all [the] king [the] these and [obj] land: country/planet their to capture Joshua beat one for LORD God Israel to fight to/for Israel
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
and to return: return Joshua and all Israel with him to(wards) [the] camp [the] Gilgal [to]

< Yoshua 10 >