< Yoshua 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
Hichejou chun Pakaiyin Joshua kommah chun aseije, “Kicha hih’in, lungthoina jong neihih’in, nasepai hochu puijinlangAi khopi khu gadelkhumtan, ajeh chu Ai lengpa le amipite, akhopi le agamchu nangma khutna kapehdoh ahitai.
2 Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
Jericho le alengpao nasuhgam banga amaho jong nasuhgam ding, amavang tuchunga hi agancha houleh anei agou nachomdoh houchu nakilah theiju ahi. Akhopiu nunglanga khun gachangpang tauvin,” ati.
3 Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
Hitichun Joshua leh asepaite chu Ai khopi gadelkhum dingin akontouvun ahi. Joshua’n asepaite lah’a galsat hatcheh sangsom thum alhengdoh’in jannin asoldoh’in,
4 akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
Hitihin thupeh aneiyin ahi: “Nangho cheuvinlang khopi nunglanga khun kinaichan gachangpang’unlang khopi delkhum dingkhun kigosademmin ummun,
5 Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
Hiteng chuleh keile kaloiho chengin khopi chu kadellutdiu chutengleh amasa-abang bangchun amaho keiho satdin hungkondoh’un tin chutengleh amaho masanga chu keiho kajamdiu ahi.
6 Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
Khopia konna chu keihon amaho chu kakidelmang sahdiu, chutengleh amahon Israelte hi amasa bang banga imasang’uva jamkitna ahitauve atidiu ahi. Chujouteng chuleh keiho amahoa konna kajam sunguva chu,
7 ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
Nangho nachangpan nauva konchun hungpotdoh’unlang akhopiu chu nalonvuh jengdiu ahi, na Pakai na Pathennun nangho khutna nahin pehdohdiu ahi.
8 Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
Chutengleh Pakaiyin nathupeh bang bangun akhopiu chu meiyin hallha jengun hichu thupeh ahi,” ati.
9 Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
Hitichun amaho akipatdoh’un Bethel leh Ai khopi lhumlam kikah achangpanna diu munnah chun ache tauvin ahi. Ahinlah Joshua chu hichejou chun mipiho toh ngahmunna chun agehkhommun ahi.
10 Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
Joshua chu jingkah langin matah’in akipatnin amite asuthouvin Ai khopi lang ajontan, hichea hin Israel upa hon ana juijun ahi.
11 Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
Joshua chu amatoh umkhom sepaiho chengchutoh khopi maija chun akijotnun sahlanga chun ngahmun asemmun ahi. Amaholeh Ai kikah’a chun phaicham khat aummin ahi.
12 Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
Chuin aman mi sang nga tobang apuijin Bethel leh Ai khopi kikah khopi lhumlamma chun achangpansah’in ahi.
13 Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
Hitichun asepai bulpi penchu khopi sahlanga apansah’in chuleh khopi lhumlamma chun changpangloi akoiyin, Joshua amatah chu phaichamma chun ageh’in ahi.
14 Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
Ai lengpan phaicham langa um Israelte chu agahmu phatnin amale asepaite jouse chun jingpitah’in Jordan phaicham gah kigalmuna munna chun anokhum tauvin ahi. Ahinla khopi nunglanga chun amaho aguh’a chaangpanga aumme tichu aman ahetlou ahi.
15 Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
Joshua leh Israel sepaite chu gallel tobang'in gammang langa chun ajamtauvin ahi.
16 Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
Hichechun khopi sunga umjouse chu akikoudoh’un abonchauvin amaho chu adeltauvin, hitichun amaho chu khopia konchun alhemdoh tauvin ahi.
17 Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
Ai ahilouleh Bethella chun mi khatcha kidalha louvin Israelte chu adelsohkei tauvin ahi. Hitichun khopi ahomkeuvin adalha tauvin ahi.
18 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
Hiche jouchun Pakaiyin Joshua komma chun hitin ahin seije, “Natengchao chu domsang’unlang Ai khopi lang ngatsah tauvin, ajeh chu keiman hichekhu nangho khutna kapehdoh ahitai” ati. Hichun Joshua’n akhutna um atengcha chu adomsang’in khopi langchu agah ngatsahtan ahi.
19 Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
Joshua’n akhut adopsang phatnin changpang ho jouse chu akiselnauva kon in ahung potdoh’un khopi langa chun alonglut jeng tauvin ahi. Amahon gangtah’in khopi chu alouvin meiyin ahallha tauvin ahi.
20 Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
Ai khomite chu akinung heijun agah veuvin ahileh, khopia konna meikhu chu vanlaijol langa akitung jengin ahileh chenading helouvin abeiden tauvin ahi. Ajeh chu Israelte gammang langa ana jamlut hochu ahung kileheijun amaho chu ahinledal tauvin ahi.
21 Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
Joshua leh Israelte chun apanlah nauchu alolhing’in khopia konchun meikhu akitungdoh tai tichu amuphatnun ahung kileheijun Ai mite chu ahin delkhum tauvin ahi.
22 Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
Alangkhatnah khopi sunga um Israelte chu ahungpotdoh’un galmi hochu anunglang uva kon in ahin delkhum uvin, hitichun Ai khopi mite chu ajet aveijuva Israelten aumchinto tauvin amaho alailunga chatmo hellin aumtauve. Israelten adelkhummun mi khat ajong asohcha ahilouleh ahingdoh’a aumpouve.
23 Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
Ai lengpa changseh chu ahingin amannun Joshua kommah ahin puilutnun ahi.
24 Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
Israel sepaiten Ai mite chu adel’uva tollhanga umjouse chu athajou phatnun amaho akinung heijun asunga langa umjouse jongchu athatchai heltauvin ahi.
25 Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
Hitichun Ai khopi sunga cheng mipite jouse, numeiti pasalti abonchan hiche nikho chun athatgam soh hellun ahileh mi sangsom le sangni alhingin ahi.
26 Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
Ai khopi sunga cheng jouse chu akisuhmanghel kahsen Joshua’n atengcha chu adomsang jing jengin ahi.
27 Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
Pakaiyin Joshua athupeh bangin, khopi sunga um agancha houleh anei agouhou chu sumang louvin Israelten amaho chandingin akichom tauve.
28 Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
Hitichun Joshua’n Ai khopi chu ahallhatan ahileh hichu tuni changgeijin amangthah paitan ahi.
29 Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
Joshua’n Ai lengpa chu nilhahlang geijin thingchungah anakhaijin, ni ahunglhum phatnin Joshua thupeh dungjuijin atahsa chu thingchunga kon in alalhauvin, khopi kelkot maija chun anaseplhauvin ahi. Amahon achunga chun song asetkhummun tuni changgeijin mutheijin aumnalaije.
30 Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
Hijouchun Joshua’n Ebal mol chungah Pakai Israel Pathen kommah maicham asemmin,
31 kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
Pakai lhacha Mose’in Israel chate anathupeh Mose daanbua anakijih bangin, thih hemma ana kikheng khalou songtum maicham chungah pumgo thilto leh chamna thilto anabollin ahi.
32 Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
Hitichun aman Israelte mitmu changtah chun Mose daan thupeh hochu song chunga chun anajihdoh’in ahi.
33 Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
Hiche jouchun Israelte jouse agam sunga pengdenho ahin khopem mi ahiuvin, upa ho jouse, vaihom ho jouse le thutanho jouse ahiuvin hopnin akihommun, hopkhat chu Gerazin mol maija adingun, hopkhat chu Ebal mol maija adingun ahi. Ahopni chun aki-angngat touvin akikah uvah Pakai kitepna thingkongpu Levi thempuho chu adingun ahi. Hichehi Israel mipiten phatthei achanna diuva Pakailhacha Mose thupeh dungjuija anaboljiu dungjuija chu abollu ahi.
34 Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
Hiche jouchun Mose’n adaan lekhabua anajihlut phatthei bohna le sapsetna hochu Joshua’n mipi ang’ah chun asimdoh’in ahi.
35 Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.
Mose thupeh thuchengho jouse chu Israel mipi ahung kikhomho leh, nunao chapangho, chuleh alah’uva cheng gamdangmi ho pumma ajahsohkei diuvin asimdoh soh hellin ahi.

< Yoshua 8 >