< Yoshua 2 >

1 Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
and to send: depart Joshua son: child Nun from [the] Shittim two human to spy silently to/for to say to go: went to see: see [obj] [the] land: country/planet and [obj] Jericho and to go: went and to come (in): come house: home woman to fornicate and name her Rahab and to lie down: lay down there [to]
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
and to say to/for king Jericho to/for to say behold human to come (in): come here/thus [the] night from son: descendant/people Israel to/for to search [obj] [the] land: country/planet
3 Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
and to send: depart king Jericho to(wards) Rahab to/for to say to come out: send [the] human [the] to come (in): come to(wards) you which to come (in): come to/for house: home your for to/for to search [obj] all [the] land: country/planet to come (in): come
4 Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
and to take: take [the] woman [obj] two [the] human and to treasure him and to say right to come (in): come to(wards) me [the] human and not to know from where? they(masc.)
5 Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
and to be [the] gate to/for to shut in/on/with darkness and [the] human to come out: come not to know where? to go: went [the] human to pursue quickly after them for to overtake them
6 (Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
and he/she/it to ascend: establish them [the] roof [to] and to hide them in/on/with flax [the] tree: stick [the] to arrange to/for her upon [the] roof
7 Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
and [the] human to pursue after them way: road [the] Jordan upon [the] ford and [the] gate to shut after like/as as which to come out: come [the] to pursue after them
8 Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
and they(masc.) before to lie down: lay down [emph?] and he/she/it to ascend: rise upon them upon [the] roof
9 akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
and to say to(wards) [the] human to know for to give: give LORD to/for you [obj] [the] land: country/planet and for to fall: fall terror your upon us and for to melt all to dwell [the] land: country/planet from face: because your
10 Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
for to hear: hear [obj] which to wither LORD [obj] water sea Red (Sea) from face: before your in/on/with to come out: come you from Egypt and which to make: do to/for two king [the] Amorite which in/on/with side: beyond [the] Jordan to/for Sihon and to/for Og which to devote/destroy [obj] them
11 Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
and to hear: hear and to melt heart our and not to arise: rise still spirit in/on/with man: anyone from face: because your for LORD God your he/she/it God in/on/with heaven from above and upon [the] land: country/planet from underneath: under
12 Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
and now to swear please to/for me in/on/with LORD for to make: do with you kindness and to make: do also you(m. p.) with house: household father my kindness and to give: give to/for me sign: indicator truth: certain
13 kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
and to live [obj] father my and [obj] mother my and [obj] brother: male-sibling my and [obj] (sister my *Q(K)*) and [obj] all which to/for them and to rescue [obj] soul: life our from death
14 Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
and to say to/for her [the] human soul: life our underneath: instead you to/for to die if not to tell [obj] word: thing our this and to be in/on/with to give: give LORD to/for us [obj] [the] land: country/planet and to make: do with you kindness and truth: faithful
15 Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
and to go down them in/on/with cord about/through/for [the] window for house: home her in/on/with wall [the] wall and in/on/with wall he/she/it to dwell
16 Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
and to say to/for them [the] mountain: mount [to] to go: went lest to fall on in/on/with you [the] to pursue and to hide there [to] three day till to return: return [the] to pursue and after to go: went to/for way: journey your
17 Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
and to say to(wards) her [the] human innocent we from oath your [the] this which to swear us
18 isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
behold we to come (in): come in/on/with land: country/planet [obj] cord thread [the] scarlet [the] this to conspire in/on/with window which to go down us in/on/with him and [obj] father your and [obj] mother your and [obj] brother: male-sibling your and [obj] all house: home father your to gather to(wards) you [the] house: home [to]
19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
and to be all which to come out: come from door house: home your [the] outside [to] blood his in/on/with head his and we innocent and all which to be with you in/on/with house: home blood his in/on/with head our if hand: power to be in/on/with him
20 Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
and if to tell [obj] word: thing our this and to be innocent from oath your which to swear us
21 Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
and to say like/as word your so he/she/it and to send: depart them and to go: went and to conspire [obj] cord [the] scarlet in/on/with window
22 Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
and to go: went and to come (in): come [the] mountain: mount [to] and to dwell there three day till to return: return [the] to pursue and to seek [the] to pursue in/on/with all [the] way: road and not to find
23 Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
and to return: return two [the] human and to go down from [the] mountain: mount and to pass and to come (in): come to(wards) Joshua son: child Nun and to recount to/for him [obj] all [the] to find with them
24 Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”
and to say to(wards) Joshua for to give: give LORD in/on/with hand: power our [obj] all [the] land: country/planet and also to melt all to dwell [the] land: country/planet from face: because our

< Yoshua 2 >