< Torati 32 >

1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema; sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.
to listen [the] heaven and to speak: speak and to hear: hear [the] land: country/planet word lip my
2 Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua, na maneno yangu na yashuke kama umande, kama manyunyu juu ya majani mabichi, kama mvua tele juu ya mimea myororo.
to drop like/as rain teaching my to flow like/as dew word my like/as rain upon grass and like/as shower upon vegetation
3 Nitalitangaza jina la Bwana. Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!
for name LORD to call: call out to give greatness to/for God our
4 Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni haki. Mungu mwaminifu ambaye hakosei, yeye ni mnyofu na mwenye haki.
[the] rock unblemished work his for all way: conduct his justice God faithfulness and nothing injustice righteous and upright he/she/it
5 Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake; kwa aibu yao, wao si watoto wake tena, lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.
to ruin to/for him not son: child his blemish their generation twisted and twisted
6 Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana, enyi watu wajinga na wasio na busara? Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu, aliyewafanya ninyi na kuwaumba?
to/for LORD to wean this people foolish and not wise not he/she/it father your to buy you he/she/it to make you and to establish: make you
7 Kumbuka siku za kale; tafakari vizazi vya zamani vilivyopita. Uliza baba yako, naye atakuambia, wazee wako, nao watakueleza.
to remember day forever: antiquity to understand year generation and generation to ask father your and to tell you old: elder your and to say to/for you
8 Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao, alipogawanya wanadamu wote, aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.
in/on/with to inherit Most High nation in/on/with to separate he son: descendant/people man to stand border people to/for number son: child Israel
9 Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake, Yakobo kura yake ya urithi.
for portion LORD people his Jacob cord inheritance his
10 Katika nchi ya jangwa alimkuta, katika nyika tupu ivumayo upepo. Alimhifadhi na kumtunza; akamlinda kama mboni ya jicho lake,
to find him in/on/with land: country/planet wilderness and in/on/with formlessness howling wilderness to turn: surround him to understand him to watch him like/as pupil eye his
11 kama tai avurugaye kiota chake, na kurukaruka juu ya makinda yake, ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka, na huwachukua kwenye mabawa yake.
like/as eagle to rouse nest his upon young bird his to hover to spread wing his to take: take him to lift: bear him upon pinion his
12 Bwana peke yake alimwongoza; hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.
LORD isolation to lead him and nothing with him god foreign
13 Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi, akamlisha kwa mavuno ya mashamba. Akamlea kwa asali toka mwambani, na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,
to ride him upon (high place *Q(k)*) land: country/planet and to eat fruit field and to suckle him honey from crag and oil from flint rock
14 kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe na kutoka makundi ya mbuzi, kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi, kwa kondoo dume wazuri wa Bashani, na kwa ngano nzuri. Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.
curd cattle and milk flock with fat ram and ram son: young animal Bashan and goat with fat kidney wheat and blood grape to drink wine
15 Yeshuruni alinenepa na kupiga teke; alikuwa na chakula tele, akawa mzito na akapendeza sana. Akamwacha Mungu aliyemuumba, na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.
and to grow fat Jeshurun and to kick to grow fat to thicken be sated and to leave god to make him and be senseless rock salvation his
16 Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni, na kumkasirisha kwa sanamu zao za machukizo.
be jealous him in/on/with be a stranger in/on/with abomination to provoke him
17 Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu: miungu wasiyoijua, miungu iliyojitokeza siku za karibuni, miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.
to sacrifice to/for demon not god God not to know them new from near to come (in): come not to know them father your
18 Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi; mkamsahau Mungu aliyewazaa.
rock to beget you to forget and to forget God to twist: give birth you
19 Bwana akaona hili, akawakataa, kwa sababu alikasirishwa na wanawe na binti zake.
and to see: see LORD and to spurn from vexation son: child his and daughter his
20 Akasema, “Nitawaficha uso wangu, nami nione mwisho wao utakuwa nini, kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka, watoto ambao si waaminifu.
and to say to hide face my from them to see: see what? end their for generation perversity they(masc.) son: child not faithful in/on/with them
21 Wamenifanya niwe na wivu kwa kile ambacho si mungu, na kunikasirisha kwa sanamu zao zisizokuwa na thamani. Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa. Nitawafanya wakasirishwe na taifa lile lisilo na ufahamu.
they(masc.) be jealous me in/on/with not god to provoke me in/on/with vanity their and I be jealous them in/on/with not people in/on/with nation foolish to provoke them
22 Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu, ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti. Utateketeza dunia pamoja na mazao yake, na kuwasha moto katika misingi ya milima. (Sheol h7585)
for fire to kindle in/on/with face: anger my and to burn till hell: Sheol lower and to eat land: country/planet and crops her and to kindle foundation mountain: mount (Sheol h7585)
23 “Nitalundika majanga juu yao na kutumia mishale yangu dhidi yao.
to snatch upon them distress: harm arrow my to end: expend in/on/with them
24 Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya, yateketezayo na tauni ya kufisha; nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu, na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.
empty famine and to feed on flash and destruction bitter and tooth animal to send: depart in/on/with them with rage to crawl dust
25 Barabarani upanga utawakosesha watoto; nyumbani mwao hofu itatawala. Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia, pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.
from outside be bereaved sword and from chamber terror also youth also virgin to suckle with man greyheaded
26 Nilisema ningewatawanya na kufuta kumbukumbu lao katika mwanadamu.
to say to cleave them to cease from human memorial their
27 Lakini nilihofia dhihaka za adui, adui asije akashindwa kuelewa, na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda; Bwana hakufanya yote haya.’”
unless vexation enemy to dread lest to alienate enemy their lest to say hand: power our to exalt and not LORD to work all this
28 Wao ni taifa lisilo na akili, hakuna busara ndani yao.
for nation to perish counsel they(masc.) and nothing in/on/with them understanding
29 Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwa aje!
if be wise be prudent this to understand to/for end their
30 Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja, au wawili kufukuza elfu kumi, kama si kwamba Mwamba wao amewauza, kama si kwamba Bwana amewaacha?
how? to pursue one thousand and two to flee myriad if: until not for rock their to sell them and LORD to shut them
31 Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu, sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.
for not like/as rock our rock their and enemy our judge
32 Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kutoka kwenye mashamba ya Gomora. Zabibu zake zimejaa sumu, na vishada vyake vimejaa uchungu.
for from vine Sodom vine their and from field Gomorrah grape their grape poison cluster gall to/for them
33 Mvinyo wao ni sumu ya nyoka, sumu yenye kufisha ya swila.
rage serpent: snake wine their and poison cobra cruel
34 “Je, hili sikuliweka akiba na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?
not he/she/it to store up with me to seal in/on/with treasure my
35 Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza. Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza; siku yao ya maafa ni karibu, na maangamizo yao yanawajia haraka.”
to/for me vengeance and recompense to/for time to shake foot their for near day calamity their and to hasten ready to/for them
36 Bwana atawahukumu watu wake, na kuwahurumia watumishi wake atakapoona nguvu zao zimekwisha wala hakuna yeyote aliyebaki, mtumwa au aliye huru.
for to judge LORD people his and upon servant/slave his to be sorry: comfort for to see: see for be gone hand: power and end to restrain and to leave: release
37 Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao, mwamba walioukimbilia,
and to say where? God their rock to seek refuge in/on/with him
38 miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji? Wainuke basi, wawasaidie! Wawapeni basi ulinzi!
which fat sacrifice their to eat to drink wine libation their to arise: rise and to help you to be upon you shelter
39 “Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye! Hakuna mungu mwingine ila Mimi. Mimi ninaua na Mimi ninafufua, Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya, wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.
to see: see now for I I he/she/it and nothing God with me I to die and to live to wound and I to heal and nothing from hand: power my to rescue
40 Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema: Hakika kama niishivyo milele,
for to lift: vow to(wards) heaven hand: vow my and to say alive I to/for forever: enduring
41 wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu, nitalipiza kisasi juu ya adui zangu na kuwalipiza wale wanaonichukia.
if to sharpen lightning sword my and to grasp in/on/with justice: judgement hand my to return: pay vengeance to/for enemy my and to/for to hate me to complete
42 Nitailevya mishale yangu kwa damu, wakati upanga wangu ukitafuna nyama: damu ya waliochinjwa pamoja na mateka, vichwa vya viongozi wa adui.”
be drunk arrow my from blood and sword my to eat flesh from blood slain: killed and captive from head leader enemy
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake, kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake, atalipiza kisasi juu ya adui zake na kufanya upatanisho kwa ajili ya nchi na watu wake.
to sing nation people his for blood servant/slave his to avenge and vengeance to return: pay to/for enemy his and to atone land: soil his people his
44 Mose na Yoshua mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia.
and to come (in): come Moses and to speak: promise [obj] all word [the] song [the] this in/on/with ear: hearing [the] people he/she/it and Hoshea son: child Nun
45 Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote,
and to end: finish Moses to/for to speak: speak [obj] all [the] word [the] these to(wards) all Israel
46 akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
and to say to(wards) them to set: consider heart your to/for all [the] word which I to testify in/on/with you [the] day which to command them [obj] son: child your to/for to keep: careful to/for to make: do [obj] all word [the] instruction [the] this
47 Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
for not word worthless he/she/it from you for he/she/it life your and in/on/with word [the] this to prolong day upon [the] land: soil which you(m. p.) to pass [obj] [the] Jordan there [to] to/for to possess: take her
48 Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses in/on/with bone: same [the] day [the] this to/for to say
49 “Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe.
to ascend: rise to(wards) mountain: mount [the] Abarim [the] this mountain: mount (Mount) Nebo which in/on/with land: country/planet Moab which upon face: before Jericho and to see: see [obj] land: country/planet Canaan which I to give: give to/for son: descendant/people Israel to/for possession
50 Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake.
and to die in/on/with mountain: mount which you(m. s.) to ascend: rise there [to] and to gather to(wards) kinsman your like/as as which to die Aaron brother: compatriot your in/on/with (Mount) Hor [the] mountain: mount and to gather to(wards) kinsman his
51 Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli.
upon which be unfaithful in/on/with me in/on/with midst son: descendant/people Israel in/on/with water Meribah (Meribath)-kadesh wilderness Zin upon which not to consecrate: consecate [obj] me in/on/with midst son: descendant/people Israel
52 Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”
for from before to see: see [obj] [the] land: country/planet and there [to] not to come (in): come to(wards) [the] land: country/planet which I to give: give to/for son: descendant/people Israel

< Torati 32 >