< Yoshua 13 >
1 Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
Joshua teh a matawng a kumcue toung dawkvah, BAWIPA Cathut ni, nang teh na matawng toe. Na la hane talai hai moi ao rah.
2 “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
Kaawm rae talainaw teh, Filistin ram hoi kamtawng teh, Geshurit ram pueng,
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
Izip ram kanîtholah Shihor palang hoi kamtawng teh, atunglah Ekron khori totouh, Kanaannaw a onae ram, Filistin siangpahrang panga touh, Gazanaw Asdodnaw, Askelonnaw, Gitnaw, Ekronnaw, Avvimnaw onae ram,
4 kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
aka lahoi kamtawng teh, Amor ram, Aphek kho totouh, Kanaan ram pueng hoi Sidon ram a tengpam kaawm e Mearah ram,
5 eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
Kanîtholah Hermon mon rahim kaawm e Baalgad kho hoi kamtawng teh, Hamath kho kâennae totouh, Gebal ram, Lebanon ram totouh ao rah.
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
Lebanon mon hoi kamtawng teh, Misrephothmaim kho totouh, mon dawk kaawm e naw hoi Sidonnaw abuemlah, Isarelnaw e a hmalah kai ni ka pâlei han. Hatdawkvah, kai ni kâ na poe e patetlah cungpam khoe sak nateh, hote talai hah Isarelnaw ram lah kârei sak.
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
Atuteh hete ram hah Isarel miphun tako touh hoi Manasseh miphun tangawn hah râw lah kârei sak.
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
Reuben miphun, Gad miphun, Manasseh miphun tangawn hah, Jordan palang kanîtholah Mosi ni raphoe awh e patetlah, namamae râw talai hah na dâw awh toe atipouh.
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
BAWIPA Cathut e san Mosi a poe e talai teh, Arnon palang teng kaawm e Aroer kho palang teng kaawm e abuemlah, khonaw hoi Dibon kho totouh, Medeba tanghling dawk kaawm e pueng,
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
Amor ram a pout totouh, Heshbon kho siangpahrang ka tawk e Ammon siangpahrang, Sihon ni a uk e khonaw pueng,
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
Gilead ram Geshurnaw, Maakathnaw onae ram, Hermon mon kaawm e pueng, Salkah ram totouh, Bashan ram pueng,
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
kalenpounge miphunnaw thung hoi kaawm rae naw, Ashtaroth kho, Edrei kho, siangpahrang ka tawk e Bashan siangpahrang, Og e uknaeram abuemlah ao awh. Hote siangpahrangnaw hah Mosi ni koung a thei teh koung a raphoe.
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
Hatei Isarelnaw ni Geshurnaw, Maakathnaw hah, pâlei awh hoeh. Hote miphunnaw teh, sahnin totouh Isarelnaw hoi rei ao awh.
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
Levih miphunnaw teh, râw poe awh hoeh. Isarelnaw e BAWIPA Cathut ni hmai hoi thuengnae naw hah, a dei pouh e patetlah ahnimae râw lah ao.
15 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
Mosi ni Reuben miphun râw a poe e ramnaw teh,
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
Arnon palang teng kaawm e, Aroer kho palang teng kaawm e khonaw hoi Medaba tanghling pueng
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
Heshbon kho hoi tanghling dawk kaawm e kho pueng, Dibon kho, Barmoth kho, Bethbaal kho,
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
Jahaz kho, Kedemoth kho, Mephaath kho,
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
Kiriathiam kho, Sibmah kho, tanghling mon dawk kaawm e Zerethsahar kho,
20 Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
Bethpeor kho, Pisgah kho, Bethjeshimoth kho,
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
tanghling dawk kaawmnaw pueng, Heshbon kho siangpahrang katawknaw, Amor siangpahrang katawknaw, Amor siangpahrang Sihon ni uknaeram abuemlah, hote siangpahrang teh a oup awh. Ahnie ram dawk kaawm e, Midian siangpahrang panga touh, Evi, Rekem, Zur, Hur, Reba hah Mosi ni a thei.
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
Profet ka tawk e Beor e capa Balaam hai a thei awh e naw hoi rei ao dawkvah, Isarelnaw ni tahloi hoi a thei awh.
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
Reuben miphun a onae hmuen a kapek awh teh, Jordan palang hoi a tengpam e pueng, Hetnaw hah Reubennaw ni a pang e khoramnaw lah ao.
24 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
Mosi ni Gad miphunnaw ama lengkaleng, râw lah a poe e ramnaw teh,
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
Jazer kho hoi kamtawng teh, Gilead kho kaawm e pueng hoi Rabbah kho e a hmalah kaawm e Roer kho totouh Ammon ram tangawn,
26 na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
Heshbon kho hoi kamtawng teh, Ramoth Mizpeh kho, Betonim kho totouh, Mahanaim kho hoi kamtawng teh, Debir kho totouh kaawm e ram,
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
Tanghling dawkvah, Bethharam kho, Bethnimrah kho, Sukkoth kho, Zaphon kho a kamtawng koehoi Jordan palang kanîtholah, Jordan palang kâkapeknae, Khinneroth, tuipui totouh, Heshbon siangpahrang, Sihon ni a uknaeram kaawm e hah pueng a poe.
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
Hetnaw heh Gad miphun lahoi râw lah a coe e khonaw lah ao.
29 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
Mosi ni Manasseh miphun tangawn râw a poe teh, Manasseh miphun tangawn ni a miphun lahoi râw lah a hmu e ramnaw teh,
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
Mahanaim kho hoi kamtawng teh, Bashan ram pueng, Bashan siangpahrang Og ni a uknaeram pueng, Bashan ram dawk kaawmnaw, Jair kho, 60 touh hah râw lah a hmu awh.
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
Gilead ram tangawn, Bashan uknaeram Og ni a uk e kho hoi, Ashtaroth kho hoi Edrei khonaw hah Manasseh e capa Makhir e catounnaw tangawn ni a miphun lahoi a tawn awh.
32 Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
Hetnaw hah Mosi ni Jordan palang kanîtholah Jeriko kho Moab tanghling dawk râw lah a rei e ramnaw lah ao.
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Levih miphunnaw teh, râw poe hoe. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA Cathut ni kâ a poe e patetlah Isarel miphunnaw e BAWIPA Cathut teh, ahnimae râw lah ao.