< Yoshua 11 >
1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Егда же услыша Иавин царь Асорск, посла ко Иоваву царю Мадонску, и к царю Семеронску и к царю Ахиавску,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
и к царем иже в Сидоне велицем и в горней, и в Араву прямо Хенерефу, и на поляну, и в Нафеддор,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
и к приморским Хананеам от восток, и к приморским Аморреом и Хеттеом, и Ферезеом и Иевусеом, иже на горе, и Евеом, и иже под Аермоном, в землю Массифа.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
И изыдоша сии и царие их с ними, людие мнози, яко песок иже при краи моря множеством, и кони и колесницы многи зело.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
И снидошася вси царие сии, и приидоша вкупе, и ополчишася при воде Маррон воевати на Израиля.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
И рече Господь ко Иисусу: не убойся от лица их, яко заутра в сей час Аз предам их язвенных пред сыны Израилевы: конем их жилы пресечеши и колесницы их да сожжеши огнем.
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
И прииде Иисус и вси людие воинстии с ним на них к воде Марронстей внезапу, и нападоша на ня в горней.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
И предаде их Господь под руце Израилевы: и секуще их, прогнаша даже до Сидона великаго и до Масрефоф-Маима и до поль Массифских к востоком: и изсекоша их, дондеже не остася в них ни един цел и избегший.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
И сотвори им Иисус, якоже заповеда ему Господь: конем их жилы пресече и колесницы их сожже огнем.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
И обратися Иисус в то время, и взя Асор, и царя его уби мечем: Асор бо бе прежде обладающий всеми царствы сими:
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
и изби все дышущее, еже в нем бысть, острием меча, и потребиша вся, и не остася в нем все дышущее: и Асор запалиша огнем.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
И вся грады царств сих и вся цари их взя Иисус и изби я мечем, и потреби их, якоже повеле им Моисей раб Господень.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Но вся грады крепки не запали Израиль, точию Асор един запали Иисус.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
И вся корысти их и вся скоты их плениша себе сынове Израилевы: людий же всех потребиша мечем, дондеже погубиша их, и не оставиша от них ни единаго дышущаго.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
Якоже повеле Господь Моисею рабу Своему, тако Моисей заповеда Иисусу: и тако сотвори Иисус, не преступи ни единаго же от всех, яже заповеда Господь Моисею.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
И взя Иисус всю землю горную и всю землю нагев, и всю землю Госомску, и равную, и яже на запад, и гору Израилеву, и поля яже при горе,
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
от горы Хелха, и яже восходит к Сеиру, и даже до Валгада, и поле Ливана под горою Аермон: и вся цари их взя и изби.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
И многи дни сотвори Иисус с цари сими брань:
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
и не бе ни единаго града, егоже не предаде Господь сыном Израилевым, кроме Евеа обитающаго в Гаваоне: всех взяша бранию:
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
яко Господем бысть укрепитися их сердцу, сопротивитися на брани противу Израиля, да потребят их, яко да не дастся им милость, но да потребятся, якоже глагола Господь к Моисею.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
И прииде Иисус в то время, и потреби (вся) Енакимы от горныя, от Хеврона и от Давира и от Анова, и от всея горы Израилевы и от всея горы Иудины, с грады их, и потреби я Иисус:
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
не остася ни един Енаким от сынов Израилевых, но точию в Газе и в Гефе и во Асидофе осташася.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
И взя Иисус всю землю, якоже заповеда Господь Моисею: и даде ю Иисус в наследие Израилю, разделением по племеном их. И преста земля воюема быти.