< Yoshua 10 >
1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
A gdy usłyszał Adonisedek, król Jerozolimski, iż wziął Jozue Haj, i zburzył je, (bo jako uczynił Jerychowi i królowi jego, tak uczynił Hajowi i królowi jego, ) a iż uczynili pokój obywatele Gabaon z Izraelem, i mieszkają w pośrodku ich;
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
Tedy się uląkł bardzo, przeto że miasto wielkie było Gabaon, jako jedno z miast królewskich, a że było większe niż Haj, a wszyscy mężowie jego waleczni.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
Przetoż posłał Adonisedek, król Jerozolimski, do Hohama, króla Hebron, i do Faran, króla Jerymota, i do Jafija, króla Lachys, i do Dabir, króla Eglon, mówiąc:
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
Przyjedźcie do mnie, a dajcie mi pomoc, abyśmy pobili Gabaonity, którzy uczynili pokój z Jozuem, i z syny Izraelskimi.
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
Zebrało się tedy, a wyciągnęło pięć królów Amorejskich, król Jerozolimski, król Hebron, król Jerymot, król Lachys, król Eglon, sami, i wszystkie wojska ich, i położyli się obozem u Gabaon, i dobywali go.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
Tedy posłali obywatele Gabaon do Jozuego, i do obozu w Galgal, mówiąc: Nie zawściągaj ręki swej od sług twoich; przyciągnij do nich rychło, a wybaw nas i pomóż nam; boć się zebrali przeciwko nam wszyscy królowie Amorejscy, którzy mieszkają po górach.
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
Ruszył się tedy Jozue z Galgal, sam i wszystek lud wojenny z nim, i wszyscy mężowie waleczni.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
(Bo był rzekł Pan do Jozuego: Nie bój się ich; albowiem w ręce twoje podałem je, a nie ostoi się żaden z nich przed tobą.)
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
I przypadł na nie Jozue nagle; bo całą noc ciągnął z Galgal.
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
I potrwożył je Pan przed obliczem Izraela, który je poraził porażką wielką w Gabaon, i gonił je drogą, którą chodzą ku Betoron, a bił je aż do Aseka i aż do Maceda.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
I stało się, gdy uciekali przed Izraelem, bieżąc z góry do Betoron, że Pan spuścił na nie kamienie wielkie z nieba aż do Aseka, i umierali; więcej ich pomarło od kamienia gradowego, niż ich pobili synowie Izraelscy mieczem.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
Tedy mówił Jozue do Pana, dnia, którego podał Pan Amorejczyka w ręce synom Izraelskim, i rzekł przed oczyma Izraela: Słońce w Gabaon zastanów się, a miesiącu w dolinie Ajalon!
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
I zastanowiło się słońce, a miesiąc stanął, aż się lud pomścił nad nieprzyjacioły swymi. Izali to nie jest napisano w księgach sprawiedliwego? Tedy stanęło słońce w pośród nieba, a nie pospieszyło się zachodzić, jakoby przez cały dzień.
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
I nie był takowy dzień przedtem, ani potem, w któryby usłuchać miał Pan głosu człowieczego, bo Pan walczył za Izraelem.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
Potem się wrócił Jozue, i wszystek Izrael z nim, do obozu do Galgal.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
A uciekło było onych pięć królów, i skryli się w jaskinią przy Maceda.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
I dano znać Jozuemu, mówiąc: Znaleziono pięć królów, którzy się pokryli w jaskini w Maceda.
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
I rzekł Jozue: Przywalcie kamienie wielkie do dziury jaskini, a postawcie u niej męże, aby ich strzegli.
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
A wy nie stójcie, gońcie nieprzyjacioły wasze, a bijcie ostatek ich, ani im dajcie uchodzić do miast ich; boć je podał Pan, Bóg wasz, w rękę waszę.
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
A gdy przestał Jozue z syny Izraelskimi bić ich porażką bardzo wielką, aż je do szczętu wytracili, a którzy żywo zostali z nich, uszli do miast obronnych;
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
Tedy wrócił się wszystek lud zdrowo do obozu, do Jozuego w Maceda, a nie ruszył przeciwko synom Izraelskim nikt językiem swoim.
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
Potem rzekł Jozue: Otwórzcie tę dziurę jaskini, a wywiedźcie do mnie tych pięciu królów z jaskini.
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
I uczynili tak, i wywiedli do niego pięciu królów onych z jaskini, króla Jerozolimskiego, króla Hebron, króla Jerymot, króla Lachys, króla Eglon.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
A gdy wywiedli one króle do Jozuego, tedy przyzwał Jozue wszystkich mężów Izraelskich, i rzekł do rotmistrzów, mężów walecznych, którzy z nim chodzili: Przystąpcie sam, a nastąpcie nogami waszemi na szyje tych królów; którzy przystąpiwszy nastąpili nogami swemi na szyje ich.
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
Zatem rzekł do nich Jozue: Nie bójcie się, ani się lękajcie; zmacniajcie się, i mężnie sobie poczynajcie; boć tak uczyni Pan wszystkim nieprzyjaciołom waszym, przeciw którym walczycie.
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
Potem pobił je Jozue, i pomordował je, i zawiesił je na pięciu drzewach, a wisieli na drzewach aż do wieczora.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
A gdy zaszło słońce, rozkazał Jozue, że je złożono z drzewa, i wrzucono je do jaskini, w której się byli skryli, a zawalono kamieńmi wielkiemi dziurę u jaskini, które tam są jeszcze i do dnia tego.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Tegoż dnia wziął Jozue Maceda, i wysiekł je ostrzem miecza, i króla ich zamordował wespół z nimi, i wszelką duszę, która była w niem; nie zostawił żadnego żywo, i uczynił królowi Maceda, jako uczynił królowi Jerycha.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
Potem ciągnął Jozue, i wszystek Izrael z nim, z Maceda do Lebny, i dobywał Lebny.
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
A podał Pan i ono w ręce Izraela, i króla jego, i wysiekł je ostrzem miecza, i wszelką duszę, która była w niem; nie zostawił w niem żadnego żywo, i uczynił królowi jego, jako uczynił królowi Jerycha.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Potem ciągnął Jozue, i wszystek Izrael z nim, z Lebny do Lachys, a położywszy się przy niem obozem, dobywał go.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
I podał Pan Lachys w ręce Izraela, i wziął je dnia drugiego, i wysiekli je ostrzem miecza, i wszelką duszę, która była w niem, tak właśnie jako uczynił Lebnie.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
Tedy przyszedł Horam, król Gazer, na ratunek Lachysowi, ale go poraził Jozue, i lud jego, tak iż nie zostawił mu żadnego żywo.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Potem ciągnął Jozue, i wszystek Izrael z nim, z Lachys do Eglon, i położyli się obozem przeciwko niemu, i dobywali go;
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
Które wziąwszy onegoż dnia, wysiekli je ostrzem miecza, i wszelką duszę, która była w niem, onegoż dnia zabił, tak właśnie jako uczynił Lachys.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
Potem się ruszył Jozue, i wszystek Izrael z nim, z Eglonu do Hebronu, i dobywał go;
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
I wzięli je, a wysiekli je ostrzem miecza, i króla jego, i wszystkie miasta jego, i wszelką duszę, która była w niem; nie zostawił żadnego żywo, tak właśnie jako uczynił Eglonowi, i wytracił je, i wszelką duszę, która w niem była.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
Stamtąd obrócił się Jozue, i wszystek Izrael z nim, do Dabir, i dobywał go.
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
I wziął je, i króla jego, i wszystkie miasta jego, i wysiekli je ostrzem miecza, i pomordował wszystkie dusze, które w niem były; nie zostawił żadnego żywo; jako uczynił Hebronowi tak uczynił Dabirowi i królowi jego, i jako uczynił Lebnie i królowi jego.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
A tak pobił Jozue wszystkę ziemię górną, i południową, i polną, i podgórną, i wszystkie króle ich; nie zostawił żadnego żywo, ale wszystkie dusze wytracił, jako mu był przykazał Pan, Bóg Izraelski.
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
I poraził je Jozue od Kades Barny aż do Gazy, i wszystkę ziemię Gosen, i aż do Gabaon.
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
A wszystkie te króle, i ziemie ich, wziął Jozue jednym razem; albowiem Pan, Bóg Izraelski, walczył za Izraelem.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
Zatem się wrócił Jozue i wszystek Izrael z nim do obozu do Galgal.