< Yoshua 10 >

1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
Or quand Adoni-tsédek, Roi de Jérusalem, eut entendu que Josué avait pris Haï, et qu'il l'avait entièrement détruite à la façon de l'interdit, ayant fait à Haï et à son Roi, comme il avait fait à Jérico et à son Roi, et que les habitants de Gabaon avaient fait la paix avec les Israélites, et étaient parmi eux;
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
On craignit beaucoup, parce que Gabaon était une grande ville, comme une ville Royale, et elle était plus grande que Haï; et [parce que] tous ses hommes étaient forts.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
C'est pourquoi Adoni-tsédek, Roi de Jérusalem, envoya vers Horam Roi de Hébron, et vers Biréam, Roi de Jarmuth, et vers Japhiah, Roi de Lakis, et vers Débir, Roi de Héglon, pour leur dire:
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
Montez vers moi, et donnez-moi du secours afin que nous frappions Gabaon; car elle a fait la paix avec Josué, et avec les enfants d'Israël.
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
Ainsi cinq Rois des Amorrhéens, [savoir], le Roi de Jérusalem, le Roi de Hébron, le Roi de Jarmuth, le Roi de Lakis, et le Roi de Héglon, s'assemblèrent et montèrent eux et toutes leurs armées, et se campèrent contre Gabaon, et lui firent la guerre.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
C'est pourquoi ceux de Gabaon envoyèrent à Josué au camp à Guilgal, en disant: Ne retire point tes mains de tes serviteurs; monte promptement vers nous, et nous garantis, et donne-nous du secours; car tous les Rois des Amorrhéens qui habitent aux montagnes, se sont assemblés contre nous.
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
Josué donc monta de Guilgal, et avec lui tout le peuple [qui était] propre à la guerre, et tous les hommes forts et vaillants.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
Et l'Eternel dit à Josué: Ne les crains point; car je les ai livrés entre tes mains, et aucun d'eux ne subsistera devant toi.
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
Josué donc vint promptement à eux; [et] monta de Guilgal toute la nuit.
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
Et l'Eternel les mit en déroute devant Israël, qui en fit un grand carnage près de Gabaon; et les poursuivit par le chemin de la montagne de Beth-horon, et les battit jusqu'à Hazéka, et jusqu'à Makkéda.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
Et comme ils s'enfuyaient de devant Israël, et qu'ils étaient à la descente de Beth-horon, l'Eternel jeta des cieux sur eux de grosses pierres jusqu'à Hazéka, dont ils moururent; et il y en eut encore plus de ceux qui moururent des pierres de grêle, que de ceux que les enfants d'Israël tuèrent avec l'épée.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
Alors Josué parla à l'Eternel, le jour que l'Eternel livra l'Amorrhéen aux enfants d'Israël, et dit en la présence d'Israël: Soleil, arrête-toi sur Gabaon, et toi Lune, sur la vallée d'Ajalon.
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
Et le soleil s'arrêta, et la lune aussi s'arrêta, jusqu'à ce que le peuple se fût vengé de ses ennemis. Ceci n'est-il pas écrit au Livre du Droiturier? Le soleil donc s'arrêta au milieu des cieux et ne se hâta point de se coucher environ un jour entier.
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
Et il n'y a point eu de jour semblable à celui-là, devant ni après, l'Eternel exauçant la voix d'un homme; car l'Eternel combattait pour les Israélites.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
Et Josué et tout Israël avec lui, s'en retourna au camp à Guilgal.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
Au reste ces cinq Rois-là s'étaient enfuis, et s'étaient cachés dans une caverne à Makkéda.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
Et on avait rapporté à Josué, en disant: On a trouvé les cinq Rois cachés dans une caverne à Makkéda.
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
Et Josué avait dit: Roulez de grandes pierres à l'entrée de la caverne, mettez près d'elle quelques hommes pour les garder.
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
Mais vous, ne vous arrêtez point, poursuivez vos ennemis, et les défaites jusqu'au dernier, [et] ne les laissez point entrer dans leurs villes; car l'Eternel votre Dieu les a livrés en vos mains.
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
Et quand Josué avec les enfants d'Israël eut achevé d'en faire une très grande boucherie, jusqu'à les détruire entièrement, et que ceux d'entr'eux qui étaient échappés se furent retirés dans les villes fermées de murailles;
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
Tout le peuple retourna en paix au camp vers Josué à Makkéda; [et] personne ne remua sa langue contre aucun des enfants d'Israël.
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
Alors Josué dit: Ouvrez l'entrée de la caverne, et amenez-moi ces cinq Rois hors de la caverne.
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
Et ils le firent ainsi, et ils amenèrent hors de la caverne ces cinq Rois: le Roi de Jérusalem, le Roi de Hébron, le Roi de Jarmuth, le Roi de Lakis et le Roi de Héglon.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
Et après qu'ils eurent amené à Josué ces cinq Rois hors de la caverne, Josué appela tous les hommes d'Israël, et dit aux Capitaines des gens de guerre qui étaient allés avec lui: Approchez-vous, mettez vos pieds sur le cou de ces Rois; et ils s'approchèrent, et mirent leurs pieds sur leur cou.
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
Alors Josué leur dit: Ne craignez point, et ne soyez point effrayés, fortifiez-vous, et vous renforcez; car l'Eternel fera ainsi à tous vos ennemis contre lesquels vous combattez.
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
Et après cela Josué les frappa, et les fit mourir, et les fit pendre à cinq potences; et ils demeurèrent pendus à ces potences jusqu'au soir.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
Et comme le soleil se couchait Josué fit commandement qu'on les ôtât de ces potences, et on les jeta dans la caverne où ils s'étaient cachés; et on mit à l'entrée de la caverne de grandes pierres [qui y sont demeurées] jusqu'à ce jour.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Josué prit aussi en ce même jour Makkéda, et la frappa au tranchant de l'épée, et défit à la façon de l'interdit son Roi et ses [habitants], et ne laissa échapper aucune personne qui fût dans cette ville; et il fit au Roi de Makkéda comme il avait fait au Roi de Jérico.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
Après cela Josué et tout Israël avec lui passa de Makkéda à Libna, et fit la guerre à Libna.
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Et l'Eternel la livra aussi entre les mains d'Israël, avec son Roi, et il la frappa au tranchant de l'épée, et ne laissa échapper aucune personne qui fût dans cette ville; et il fit à son Roi comme il avait fait au Roi de Jérico.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Ensuite Josué et tout Israël avec lui passa de Libna à Lakis, et se campa devant elle, et lui fit la guerre.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
Et l'Eternel livra Lakis entre les mains d'Israël, qui la prit le deuxième jour, et la frappa au tranchant de l'épée, et toutes les personnes qui étaient dedans, comme il avait fait à Libna.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
Alors Horam Roi de Guézer monta pour secourir Lakis; et Josué le frappa, lui et son peuple, de sorte qu'il n'en laissa pas échapper un seul homme.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Après cela Josué et tout Israël avec lui passa de Lakis à Héglon; et ils se campèrent devant elle, et lui firent la guerre;
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
Et ils la prirent ce jour-là même, et la frappèrent au tranchant de l'épée; et [Josué] défit à la façon de l'interdit en ce même jour-là toutes les personnes qui y étaient, comme il avait fait à Lakis.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
Puis Josué et tout Israël avec lui monta d'Héglon à Hébron, et ils lui firent la guerre.
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
Et ils la prirent, et la frappèrent au tranchant de l'épée, avec son Roi, et toutes ses villes, et toutes les personnes qui y étaient; il n'en laissa échapper aucune, comme il avait fait à Héglon; et il la défit à la façon de l'interdit, et toutes les personnes qui y étaient.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
Ensuite Josué et tout Israël avec lui rebroussa chemin vers Débir, et ils lui firent la guerre.
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
Et il la prit avec son Roi, et toutes ses villes; et ils les frappèrent au tranchant de l'épée, et défirent à la façon de l'interdit toutes les personnes qui y étaient; il n'en laissa échapper aucune. Il fit à Débir et à son Roi comme il avait fait à Hébron, et comme il avait fait à Libna et à son Roi.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
Josué donc frappa tout ce pays-là, la montagne, et le Midi, et la plaine, et les pentes des montagnes, et tous leurs Rois; il n'en laissa échapper aucun; et il défit à la façon de l'interdit toutes les personnes vivantes, comme l'Eternel le Dieu d'Israël l'avait commandé.
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
[Ainsi] Josué les battit depuis Kadès-barné jusqu'à Gaza, et tout le pays de Gosen, jusqu'à Gabaon.
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
Il prit donc tout à la fois ces Rois-là et leur pays; parce que l'Eternel, le Dieu d'Israël, combattait pour Israël.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
Après quoi Josué et tout Israël avec lui s'en retournèrent au camp à Guilgal.

< Yoshua 10 >